Printer za picha (Mini lab)

Fedora

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2013
Posts
238
Reaction score
173
Wadau nataka kufungua ofisi (photo studio) na nimekua kwenye mazungumzo na jamaa yangu ambae yeye ni mzoefu wa biashara hii kwa muda mrefu nikimuomba aniuzie printer yake (noritsu 3001) ambayo kwa sasa haitumii baada ya kununu nyingine kubwa. Tulikubaliana mil. 6 Lakini tangu tufanye makubaliano hayo amekua hanipi ushirikiano mzuri kwa kutopokea simu zangu ili tufanye taratibu za kulipana na kukabidhiana mzigo, hivyo nataka kuachana nae. Naombeni msaada ni wapi hapa tanzania naweza kupata printer za picha (minilab) kama hiyo kwa bei rafiku.

Nawasilisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sorry kwa kutoka nje ya mada, ivi biashara ya kusafisha picha bado inalipa. Maana naona imepoa sana siku za hivi karibuni kuna wahindi walikuwa na branch kibao karibu nchi nzima wamefunga wamehamia zao Canada kuna jamaa yangu kafanya nao kazi miaka kama 10 hivi karudi zake Moshi baada ya Wahindi kufunga. Mimi naona kama una pesa nzuri jaribu kwenye mashine kubwa za mabango naona kama upepo umehamia huko.
 
Ni kweli kwa maeneo ya mjini biashara hii imepungua sana hasa kutokana na kupungua kwa street photograph kulikochangiwa na kuja kwa smart phone, lkn kwa maeneo ya vijijini biashara bado ipo, japo ni ya msimu, hasa wakati wa sikukuu na matukio makubwa kama harusi, ubatizo, misiba nk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Me naulizia zile mashine ndogo za kuprint picha portable ambazo wapiga picha huwa wanatembea nazo na kuprint pcha papo hapo

Mwenye kuzifaham bei yake naomba anijuze wakuu

Sent using My phone
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…