Kasinja jr
JF-Expert Member
- Aug 4, 2017
- 1,057
- 1,932
Mbona zako.ni robo ya polepole hujajinyonga?Nikiwa na akili kama ya Pole Pole bora nifupishe maisha kwa sababu naidhalilisha hata familia
Ccm ina tabia ya kuwaharibu wasomi wa nchi hii, tazama walivyomharibu lipumba na mutungiCCM haijawahi kumuacha mtu na akili zake
Kumbe CCM inaishi kwa awamu (matumaini) V! Nchi haiwezi kuendelea chini ya mfumo usio endelevu.USAHIHI NA UHALALI WA SERA NA MSIMAMO WA CCM
Mnamo mwezi wa April 2017, Kabla ya Majadiliano na Barrick walisema kwa kuzuia makinikia tutashtakiwa na kushinikiza tuachane na jambo hilo.
Ilipofika kwenye mwezi wa Julai 2017, tukaendelea kusimama imara na kuwapuuza, Mtendaji wa Barrick akaja na kukiri makosa na kukubali lazima Tanzania ipate haki yake katika uchimbaji madini. Wapinzani wakasema sio kweli na hatukuelewa kiingereza cha Bwana Thornton. Tuliwapuuza na tukaanza majadiliano kwa umakini mkubwa, kwasababu hawakujua mazungumzo yalikuwaje, wakazusha kwamba ngoma nzito, na eti majadiliano yamekwama.
Leo Mwezi wa Oktoba 2017, Majadiliano yameisha na Mtendaji wa Barrick amesema haya ni makubaliano bora zaidi kuingiwa huenda Duniani. Tanzania inapata gawio la umiliki migodi asilimia 16 na itapata gawio la faida baada ya kodi zote kukatwa la asilimia 50 na Barrick asilimia 50.
Maana yake ni 16% + 50% ya faida + Kodi zote kwa mujibu wa sheria + Bilioni 700 za awali na Mazagazaga mengine kibao kwa watanzania.
Wapinzani mufilisi wanasema eti tukatae twende Mahakamani.
Tumewashtukia, tumewang'amua mnataka kutuchezesha ngoma ya kitoto ilhali sie watu wazima.
Kwa Serikali ya CCM, Endeleeni kuchapa kazi maana 2020 tutatoa hesabu kwa ushahidi, hawa jamaa wa kuzungusha ngumi na vidole uma hawana cha kupoteza
Rais Magufuli ameshaelekeza kufumua pia maeneo mengine ya madini katika Almasi na Tanzanite ili kuhakikisha kila haki ya watanzania inapatikana. Najua katika mchakato na vita hii tutakanyaga vidole vya baadhi ya watu tunafanya kwa nia njema na maslahi mapana ya watanzania.
Waendelee kuzungusha ngumi wakati sisi tukizungusha gurudumu la Maendeleo ya Taifa, wakati wao wakinyoosha vidole sisi tupambane kunyoosha nidhamu ya Nchi na hasa kwa watumishi na Viongozi wetu.
Ukombozi wa Kiuchumi ni Sera ya CCM Awamu ya V na ni hakika
Ndg. John Pombe Joseph Magufuli watanzania wamekuamini simamia haki zao, unaacha alama kubwa katika maisha ya wananchi wa kawaida, utabarikiwa hapa duniani na mbinguni, komaa baba, sisi watu wa kawaida tuko nawe na tunaona matunda ya kazi zako.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
USAHIHI NA UHALALI WA SERA NA MSIMAMO WA CCM
Mnamo mwezi wa April 2017, Kabla ya Majadiliano na Barrick walisema kwa kuzuia makinikia tutashtakiwa na kushinikiza tuachane na jambo hilo.
Ilipofika kwenye mwezi wa Julai 2017, tukaendelea kusimama imara na kuwapuuza, Mtendaji wa Barrick akaja na kukiri makosa na kukubali lazima Tanzania ipate haki yake katika uchimbaji madini. Wapinzani wakasema sio kweli na hatukuelewa kiingereza cha Bwana Thornton. Tuliwapuuza na tukaanza majadiliano kwa umakini mkubwa, kwasababu hawakujua mazungumzo yalikuwaje, wakazusha kwamba ngoma nzito, na eti majadiliano yamekwama.
Leo Mwezi wa Oktoba 2017, Majadiliano yameisha na Mtendaji wa Barrick amesema haya ni makubaliano bora zaidi kuingiwa huenda Duniani. Tanzania inapata gawio la umiliki migodi asilimia 16 na itapata gawio la faida baada ya kodi zote kukatwa la asilimia 50 na Barrick asilimia 50.
Maana yake ni 16% + 50% ya faida + Kodi zote kwa mujibu wa sheria + Bilioni 700 za awali na Mazagazaga mengine kibao kwa watanzania.
Wapinzani mufilisi wanasema eti tukatae twende Mahakamani.
Tumewashtukia, tumewang'amua mnataka kutuchezesha ngoma ya kitoto ilhali sie watu wazima.
Kwa Serikali ya CCM, Endeleeni kuchapa kazi maana 2020 tutatoa hesabu kwa ushahidi, hawa jamaa wa kuzungusha ngumi na vidole uma hawana cha kupoteza
Rais Magufuli ameshaelekeza kufumua pia maeneo mengine ya madini katika Almasi na Tanzanite ili kuhakikisha kila haki ya watanzania inapatikana. Najua katika mchakato na vita hii tutakanyaga vidole vya baadhi ya watu tunafanya kwa nia njema na maslahi mapana ya watanzania.
Waendelee kuzungusha ngumi wakati sisi tukizungusha gurudumu la Maendeleo ya Taifa, wakati wao wakinyoosha vidole sisi tupambane kunyoosha nidhamu ya Nchi na hasa kwa watumishi na Viongozi wetu.
Ukombozi wa Kiuchumi ni Sera ya CCM Awamu ya V na ni hakika
Ndg. John Pombe Joseph Magufuli watanzania wamekuamini simamia haki zao, unaacha alama kubwa katika maisha ya wananchi wa kawaida, utabarikiwa hapa duniani na mbinguni, komaa baba, sisi watu wa kawaida tuko nawe na tunaona matunda ya kazi zako.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Magufuli ni level nyingine muda utaongea, kama issue ya madini ameiweza basi hatashindwa na kitu chochote tumpe ushirikiano tu Tanzania itafika mbali.
Kwani lowassa na Sumaye ni wanaCCM kwa sasa?Kwani walioingia hiyo mikataba ni wapinzani, ni hao hao maccm sasa upinzani unaingiaje hapo, maccm bhana sijui yakoje
Kwa nini mkalimani alizuiliwa na rais asitafsiri maneno ya kabudi kwa kiingereza na mzungu naye akasikia maana yake ni nini ccm munaangalia wapinzani hamjui tupo tusio na vyama hatumjui zito wala mbowe na hatujui ccm ni Kitu gani hatujasikia hatima ya makinikia tunasikia mambo mengine kabisamuelewe tusio na vyama tuna maamuzi zaidi yenu munaokula na kulala ndani ya siasa hatima ya taiga hili so yenu nyie tumewaamini tu OK muda utaongeaUSAHIHI NA UHALALI WA SERA NA MSIMAMO WA CCM
Mnamo mwezi wa April 2017, Kabla ya Majadiliano na Barrick walisema kwa kuzuia makinikia tutashtakiwa na kushinikiza tuachane na jambo hilo.
Ilipofika kwenye mwezi wa Julai 2017, tukaendelea kusimama imara na kuwapuuza, Mtendaji wa Barrick akaja na kukiri makosa na kukubali lazima Tanzania ipate haki yake katika uchimbaji madini. Wapinzani wakasema sio kweli na hatukuelewa kiingereza cha Bwana Thornton. Tuliwapuuza na tukaanza majadiliano kwa umakini mkubwa, kwasababu hawakujua mazungumzo yalikuwaje, wakazusha kwamba ngoma nzito, na eti majadiliano yamekwama.
Leo Mwezi wa Oktoba 2017, Majadiliano yameisha na Mtendaji wa Barrick amesema haya ni makubaliano bora zaidi kuingiwa huenda Duniani. Tanzania inapata gawio la umiliki migodi asilimia 16 na itapata gawio la faida baada ya kodi zote kukatwa la asilimia 50 na Barrick asilimia 50.
Maana yake ni 16% + 50% ya faida + Kodi zote kwa mujibu wa sheria + Bilioni 700 za awali na Mazagazaga mengine kibao kwa watanzania.
Wapinzani mufilisi wanasema eti tukatae twende Mahakamani.
Tumewashtukia, tumewang'amua mnataka kutuchezesha ngoma ya kitoto ilhali sie watu wazima.
Kwa Serikali ya CCM, Endeleeni kuchapa kazi maana 2020 tutatoa hesabu kwa ushahidi, hawa jamaa wa kuzungusha ngumi na vidole uma hawana cha kupoteza
Rais Magufuli ameshaelekeza kufumua pia maeneo mengine ya madini katika Almasi na Tanzanite ili kuhakikisha kila haki ya watanzania inapatikana. Najua katika mchakato na vita hii tutakanyaga vidole vya baadhi ya watu tunafanya kwa nia njema na maslahi mapana ya watanzania.
Waendelee kuzungusha ngumi wakati sisi tukizungusha gurudumu la Maendeleo ya Taifa, wakati wao wakinyoosha vidole sisi tupambane kunyoosha nidhamu ya Nchi na hasa kwa watumishi na Viongozi wetu.
Ukombozi wa Kiuchumi ni Sera ya CCM Awamu ya V na ni hakika
Ndg. John Pombe Joseph Magufuli watanzania wamekuamini simamia haki zao, unaacha alama kubwa katika maisha ya wananchi wa kawaida, utabarikiwa hapa duniani na mbinguni, komaa baba, sisi watu wa kawaida tuko nawe na tunaona matunda ya kazi zako.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Nenda argentina ukaangalie mikataba yao...Polepole, hizi balimi saba tunywe huku tukisubiri Noah au ndio tunywe tukalale?
Alafu mbona niko bar na wananiambia siwezi pata balimi hata moja kwakuwa hela hamna. Ila nyie lakini ....!
Inamaana hakuna kilichopatikana kabisa?
Halafu ni accounts za wapi unakuwa na hisa 16% , upate gawio la hiyo 16% na 50% ya faida bila sababu za msingi?
Polepole elewa kiingereza, 'too good 'is not good at all , actually, it is bad.
Au uliingia na hiyo sura yako ya ajabu kwenye majadiliano wazungu wakaogopa?