Pinda amfunza Makamu wa Rais unywaji pombe ya kifipa



sababu ya tanganyika kuendelea na muungano wa zanzibar ndo kama hii kudumisha mila na desturi za kibantu na kuondokana na ule ukiritimba wa kimanga wanaofanyiwa wabantu wenzetu huko visiwani

Nilishika kikombe cha chai, umeniumiza mbavu hadi chai kunimwagikia, mambao haya ya wakuu wetu yanafikirisha zaidi ya kuchekesha.

Niambieni hapo angefanya hivyo mheshimiwa Mbowe, Zito, Mnyika, Dr. Slaa magazeti yangepamba habari hiyo na gazeti la Uhuru lingetoa habari hiyo kwa mwezi mzima. Lakini kwa hawa magamba wanafanya jitihada zote kuzima isijulikane.
 

Nimepita pale getini Katavi juzi nikiwa peke yangu na drive hakuna kilichotokea, na sasa hivi nipo Mlowo.

Kuhusu Nguruwe na Bangi, hapo nadhani unajichanganya kama si kuchanganya mambo. Bangi ni haramu kwa mujibu wa sheria za nchi na mtu hatakiwi kuitumia by any means, wakati Nguruwe ni haramu kwa mujibu wa sheria za kiimani na unaruhusiwa kula kidogo kama una njaa.
 
Hiyo inaitwa Chimpumu,kwa kawaida hutiwa maji ya moto na majivu kidogo( kwa kifipa nyau) kama hujahahi kuinywa usijaribu ni kali kweli kweli. Si inaona mh. kijasho kinamtoka.
 
Huyo pinda anamfanyanini mzee wa watu asije anza kucheza kiduku :lol:
 

Bangi nimeiingiza hapa katika maana ya kujenga hoja ya mmoja alivyotetea utamaduni. Kuna makabila ya kanda fulani yana mapokea ya kutumia bangi kama kikolezo (kiungo) kwenye mboga za majani. Kwa sababu ya bangi kuharamishwa matumizi yake ipo siku kiongozi wa kitaifa akifika maeneo ambayo yana mapokeo ya kutumia bangi basi tutatetea kulinda utamaduni kwa vile watu hao wana utamaduni wa kutumia bangi? Kuhusu la kuvuka geti la Katavi lisikuumize kichwa maana hapa manju anaporidhia audience kuna kitu kinachoitwa pambizo ili kusisimua ukumbi.
 
Kumbe ndo mana macho ya Pinda yako vile yalivyo, Chimpumu si mchezo nduguzanguni
 


Kumbe ndo mana macho ya Pinda yako vile yalivyo, Chimpumu si mchezo nduguzanguni

Umeona ehe! kadiri ya picha hiyo Pinda kisha anza kuonja yupo ulimwengu mwingine, hata hajitambui kwani mkorogo huo uliandaliwa rasmi kuwaweka sawa.
 

Kuwa Kiongozi haikufanyi upoteze the social part of yourself. Nani amekwambia kwamba ukiwa kiongozi ndo usinywe pombe na wanakijiji wenzio? Cha msingi hapa ni kuwaelekeza wajue muda gani wa kunywa pombe na muda gani wa kufanya kazi. Tusipende kuishi maisha ya kuigiza (artificial life) eti kwa vile wewe ni kiongozi ndo usinywe na kufurahia kinywaji na wananchi.....
 



Utetezi wako dhaifu, hali hii wamejidhalilisha sana ndio maana vyombo vya habari vimewalinda kutotoa habari hii. Vyombo vichache vimechakachua na kutoa picha fulani ambayo haionyeshi wanavyokuywa pombe katika mkutano wao. Ni jambo la kushangaza serikali kupanga ratiba ya Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kuwa na tukio la kwenda kunywa pombe huko mkoani Katavi? Tuna mambo mengi ya kuhangaika ambayo taifa limezama kwenye umaskini sasa wakuu wa nchi wanajiliwaza na kuchochea ulevi wazi wazi na hadharani, hapa tukubaliane bila utetezi bali kizalendo kwamba wameteleza. Wanapashwa kujirekebisha sana tu na inatakiwa waliombe radhi taifa na wananchi kwa kuonyesha mfano mbaya.
 
Mtu ni afya haya ni mambo ya kale sana




Licha ya mtu ni afya au mambo ya kale, lakini cha aibu serikali kupanga ratiba ya viongozi wake kitaifa kwenda huko mikoani kunywa pombe hadharani kwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Waziri Mkuu kushiriki na kuhamasisha ulevi serikali imejidhalilisha mno. Ni dalili tosha kuhamasisha ulevi badala ya kuhamasisha watu uwajibikaji. Busara ingetanguliwa katika hili Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wasingepata nafasi ya kujidhalilisha hivyo. Washauri wao nao wamewategea mtego nao bila kutumia vizuri bongo zao wameingia kichwa kichwa.

Kikwete mwenyewe ameshaingia kwenye mitego kama hii mara kadhaa kufungua mahoteli na kadhalika, ina maana hata mwenyewe hatumii vizuri ubongo vinginevyo kurudia kosa juu ya kosa ni udhaifu.
 
Hiyo pombe ya kuinamia kwenye chungu namna hiyo, madhara ni kuwa ukishamaliza kunywa macho yanaanza kutaka kutoka nje kama mjusi aliyebanwa na mlango. Stop drinking that thing near the pot with your eyes open, lol!!
 

Sasa wewe shule umefuata nini kama unaandika pumba kama hizi. Kutumia pombe ya kienyeji na jinsi ya kuinywa ni vitu viwili tofauti. Kinachokera hapa sio kunywa hiyo pombe ya asili lakini jinsi inavyonywewa kwa kutumia mirija ambayo ina uwezekano wa kuvuta pombe kutoka kwenye chombo na kurudisha mabaki kwenye chombo hicho hicho ni hatari sana kwa afya za watumiaji.

Ndiyo maana mnakwenda shule kuelimishwa mambo kama hayo na ningetegemea wewe msomi kuwaelimisha wengine juu ya madhara yanayoweza kuwapata watumiaji wa pombe hiyo kwa mtindo huo.

Kwa namna nyingine hao waheshimiwa hapo walitakiwa kuwa mfano kuwaelimisha hao ndugu zao waliotoka huko walikotoka juu ya madhara ya kutumia mirija hiyo kwa pamoja kwenye chombo kimoja. Kama ni lazima watumie mirija basi kila mtu awe na chombo chake.
 
semeni ha hii sasa


We mchokozi, kwani muziki wa mdundiko ambao ndio kibwagizo kinacho konga nyoyo za watu hadi kuwa na mvuto mkubwa kwa watoto kufikia hatua ya kupotea wasijue walikotokea sababu ya kufuata mdundiko ni ishara za mkulu kuwa na mvoto kwa kuchangamsha hadhara kwa stretch za rap? Hapa naona pinda ni kujifunza tu maana rap si ngoma ya asili yake, ila mkulu ndo zake maana amekua akiiona na kucheza.

Ngoma ya mdundiko hakuna pombe ya machicha au komoni/kimpumu na pengine mbege, sidhani kama Pinda atastahimili, maana anahitaji nerves ziwe stimulated by alcohol hapo anaweza kuchamnkia microphone.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…