Habari za Jumamosi wana JF karibuni tena kwenye makala nyingine fupi, leo tutaenda kuangalia jinsi ya kuongeza ulinzi wa simu yako ya android kwa aina mpya ya lockscreen.
Najua wengi wetu tumesha zoea kuwa na ulinzi wa aina flani kwenye simu zetu, lakini kifupi ni kwamba inawezekana kwa sasa unaona ulinzi ulio nao kwenye simu yako hautoshi hivyo unataka kuongeza aina flani ya ulinzi ambayo ni ngumu mtu kujua au kugundua namna ya kufungua simu yako hivyo basi hii ikiwa ndio sababu leo Tanzania Tech tunakuletea aina hii mpya ya lock Screen ambayo na uhakika itakuwa ni ongezeko zuri na bora kwenye ulinzi wa simu yako.