Shinbet18
JF-Expert Member
- Jan 17, 2018
- 255
- 252
Habari za jioni wandugu wote humu ndani.Baada ya pilika zote za kutafuta mwenza wa maisha hatimae nimeangukia Kwa bint wa kisambaa kutoka Kauzeni Maramba Tanga.
Nilikotoka ilikuwa vita ya isiyoisha kila siku sitataja kabila la mke wa awali.Nilibanikwa roho ikauma kila sekunde mpaka nikadhoofu.
Baada ya kupata kimwana mweupe bila mkorogo umbo kama la Shunie nahisi kama kupaa.Mipango mingi iliyovurugika inarudi vema kila siku kama Christmas.
Bint ni mpole sio mkali mpaka namchokoza angalau aongee nione dimpoz za kisambaa macho yake goroli meno meupe yaliyo takaswa kwa maji ya milima ya usambara.
Naulizwa kama nataka kwenda kuoga ya moto au baridi ananisugua na brash la dodoki huko bafuni nafutwa maji na taulo linalonukia namwambia asante mke wangu.
Nachuliwa mgongo nirudipo safarini kabla ya kuandaliwa magimbi ya nazi niyapendayo sana.
Sitamaliza jamani sifa zake nimeona nishee nanyi raha nipatazo.
Nilikotoka ilikuwa vita ya isiyoisha kila siku sitataja kabila la mke wa awali.Nilibanikwa roho ikauma kila sekunde mpaka nikadhoofu.
Baada ya kupata kimwana mweupe bila mkorogo umbo kama la Shunie nahisi kama kupaa.Mipango mingi iliyovurugika inarudi vema kila siku kama Christmas.
Bint ni mpole sio mkali mpaka namchokoza angalau aongee nione dimpoz za kisambaa macho yake goroli meno meupe yaliyo takaswa kwa maji ya milima ya usambara.
Naulizwa kama nataka kwenda kuoga ya moto au baridi ananisugua na brash la dodoki huko bafuni nafutwa maji na taulo linalonukia namwambia asante mke wangu.
Nachuliwa mgongo nirudipo safarini kabla ya kuandaliwa magimbi ya nazi niyapendayo sana.
Sitamaliza jamani sifa zake nimeona nishee nanyi raha nipatazo.