MAHOJIANO MAALUMU NA NAIBU KATIBU MKUU WA NRA
Ndugu wana-Mzizima 24, mtakumbuka kuwa nchi yetu iliingia katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 wakati wa utawala wa awamu ya pili ya Mzee wetu, Al-Haj Ali Hassani Mwinyi.Ni katika kipindi hicho ambapo mabadiliko kadhaa yalifanyika kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuruhusu urejeshwaji wa mfumo huo. Ni hapo ndipo vyama kadhaa vilisajiliwa na mwaka 1995 Tanzania ikafanya uchaguzi mkuu chini ya mfumo huu mpya.
Mpaka sasa Tanzania imefanya uchaguzi mara nne chini ya mfumo huu mpya, na inakadiriwa kuwepo kwa vyama vya kisiasa visivyopungua 22.
Miongoni mwa vyama vya mwanzo kabisa baada ya kutambulishwa kwa mfumo huu, ni chama cha NATIONAL RECONSTRUCTION ALLIANCE (NRA), kilichoasisiwa mwaka 1992 chini ya mwenyekiti wake wa kwanza, hayati ndugu Aboubakar Ulotu, na baadaye chini ya hayati ndugu Kighoma Ali Malima.
Katika kujadili historia, hatima, sera na miongozo ya chama hiki kikongwe na siasa cha nchi yetu kwa ujumla tumemualika ulingoni NAIBU KATIBU MKUU wa chama hiki kwa upande wa Tanzania Bara, ambaye pia ni Katibu wa Bodi ya Wadhamini wa Chama hiki, ndugu Hassan Kisabya Almas.
Ndugu Kisabya ni miongoni mwa viongozi vijana katika nafasi za juu za kisiasa hapa nchini akiwa na umri wa miaka 29, nafasi inayomfanya awe kielelezo cha uwezo wa vijana kisiasa.
Tunawakaribisha wasomaji wetu katika mahojiano haya maalumu na mnaruhusiwa kumuuliza ndugu Kisabya naye atakuwa tayari kuwajibu.
https://sw-ke.facebook.com/mzizima24/posts/535871183163797