punainen-red
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 1,731
- 450
Jamani ww kaka mbona unapata tabu bure,huyo dada wa watu keshakwambia nakupenda na anatimiza wajibu wake bila kujali umbali uliopo na pamoja na kujua una mchumba still amepata ujasiri wa kukueleza la moyon bado tu unaulizia cha kufanya na huyo anayekutafuta wakati wa shida zake,fungua macho yako usipoteze mda mpe nafasi anayekupenda acha kumbembeleza huyo asiyojua thaman ya penzi lako.
habari zeni Great thinkers, Naanza kama ifuatavyo, Kitambo niliwahi kuomba msaada kupitia Jamvi hili kuhusu Mchumba wangu.
Mimi ni kijana wa Kiume Nilieko Ughaibuni na nilimchumbia Msichana mmoja baada ya kukubaliana, ingawa mwanzo alikuwa na whats so called "sitaki nataka".
Sasa tatizo lipo kwenye mawasiliano maana mimi ndo nipige simu kila wiki na kama sikupiga basi ndo haniulizi naweza kukaa wiki 3 nisipate hata sms 1. nikimuuliza oo simu haina credits, oo mara sim mbovu. Ila akiwa na shida ya kitu lazima atatuma sms na kwa namba hiohio yake. Mama yake aliniambia kweli sim ya mwanawe ina matatizo kweli na namuamini kwa hilo.
Kinachoniumiza na kujiuliza je kweli inawezekana mtu mchumba wake asiwasiliane nae hata sms kwa sim ya mtu mwengine kama ya Mama yake au Baba ake. Nahisi hana feelings kwangu au Mnanisaidiaje Kwa hili?
Jengine ni kwamba nilikuwa na mahusiano au urafiki na msichana mmoja hukohuko Tanzania kabla sijaondoka ila nilikuwa nikiyaona ya kawaida tu,
Kumbe Mwenzangu alikuwa na hisia za Kimapenzi kwangu kwani nilikuja kugundua wakati nishafika huku Ughaibuni, alinimkia mwenyewe baadae baada ya kujua nina mchumba tayari. Lakini anawasiliana nami kila siku ya Mungu mpaka naanza kumuonea huruma Kwa bidii yake.
Hebu jamani nipeni ushauri hapa maana sijui niamue nini mpaka sasa.
tafuta msichana huko huko hawa wa huku wako kimaslahi zaidi,tena huyo anayejua una galfriend na uko ughaibuni muogope.mwizi huyo kamata
mwizi meeeeeeeeeeeeeeeeeeeeen!
hujasema huyo galfriend wako ana kazi yenye kumuingizia kipato????inawezekana kweli anataka kuwasiliana na wewe sema hela hana,kama vipi uwe unamtumia hivyo vidola sijui pounds uone kama hawasiliani na wewe.....kusema ule ukweli mie ningewabwaga wote wawili ningerudi na mzungu....
Piga chini mwenyewe nilikuwa naye kama huyo nikaona ananipotezea time hana future,penda ulipopendwa,waambie hata kama kujaribiwa syo hvyo,hata muonja nyama huonja kipande syo unasema unaonja huku unamaliza nyama nzima.
Hebu mnunulie simu banaa! Halafu baada ya wiki mbili akwambie imedumbukia kwenye maji! Mnarudi kulekule kwenye simu mbovu. Inaonyesha umependa sana kaka kwamba bila yeye hakuna maisha?! Nachukia sana mtu anapokubali kuchezewa akili kizembe hivyo. Kwani unashindwa nini kumpa live huyo binti?! Agggggrrrrrrrrrh.
fais buku keshatangaza dau mjibu basi
kama uko USA wabongo wazuri wapo huko huna haja ya kuhangaika
leave the two girls in bongo wote hawaeleweki
inaonekana ninyi nyote amjapendana,kwani naona unataka kuamia kwa huyo dada mwingine kwa sababu kuwa mpenzi wako wa mwanzo aeleweki,lakini hicho sio kigezo inabidi mkutane na inabidi wawe wazazi wa pande zote mbili muyaongee kama itashindika ndyo ufikilie kwa mwanamke mwingine
Huyu mdada hayuko tayari kwasababu dada zetu wanavyopenda wachumba wanaoishi usa kama yuko chuo kila mtu atajua ana mchumba usa na huwa wanaonyesha sms na simu wanazopiga na wanazopigiwa, huyu wako ni tatizo tafuta m bongo hukohuko