Kwa Zanzibari tunasubiri siku 90 uchaguzi mwingine ufanywe, kama Maalim Seif alishinda kihalali basi atashinda tena kihalali. tatizo naloliona ni kwamba wanasiasa hawana tatizo na wanacheka pamoja, ila mashabiki wao ndio wanaotaka kuleta matatizo kama Makongoro alivyosema awali.
Imewekwa wazi kuwa CCM haijawahi kushinda uchaguzi mkuu Zanzibar tangia 1995. Nimesoma Mzee Moyo aliweka hilo wazi kuwa Yeye ndio alimfuata Seif akubali "kushindwa" kwa sababu CCM hawana mpango wa kuacha kung'ang'ania madaraka. Kwa hiyo tatizo sio kama Seif alishinda, tatizo ni kuwa CCM wameshashindwa mara inne na hii ni ya tano.Kwa Zanzibari tunasubiri siku 90 uchaguzi mwingine ufanywe, kama Maalim Seif alishinda kihalali basi atashinda tena kihalali. tatizo naloliona ni kwamba wanasiasa hawana tatizo na wanacheka pamoja, ila mashabiki wao ndio wanaotaka kuleta matatizo kama Makongoro alivyosema awali.
Imewekwa wazi kuwa CCM haijawahi kushinda uchaguzi mkuu Zanzibar tangia 1995. Nimesoma Mzee Moyo aliweka hilo wazi kuwa Yeye ndio alimfuata Seif akubali "kushindwa" kwa sababu CCM hawana mpango wa kuacha kung'ang'ania madaraka. Kwa hiyo tatizo sio kama Seif alishinda, tatizo ni kuwa CCM wameshashindwa mara inne na hii ni ya tano.
Tatizo si mashabiki, Tatizo ni CCM na Tume isiyo huru ya uchaguzi.
CCM inang'ang'ania madaraka na Tume haitendi haki.
NEC wameiwezesha CCM kwa upande wa bara na ZEC walitegemea kuiwezesha CCM Zanzibar. Seif aliweza kukusanya matokeo yaliyobandikwa vituoni mapema na kuweka wazi kitu kilichoweza kuifunga mikono ZEC isiweze kuchakachua na kuiwezesha CCM.
Kurudia uchaguzi sio tu ni ufujaji wa fedha za umma na wafadhili lakini pia ni ubakaji wa demokrasia wenye nia ya kuibakisha CCM madarakani.
Zinahitajika billioni 12 ili kurudia uchaguzi.
kikwete si amirijeshi mkuu
CCM walishasema nchi haiwezi kuchukuliwa kwa karatasi. Msikilize hapa Asha Bakari akimwaga sera ya CCM: www.youtube.com/watch?v=nQW3VP1W5hU
Wao wana sera inayosema "Mapinduzi daima". Kilichotokea Zanzibar ni mapinduzi. Uchaguzi utarudiwa na watahakisha "wanashinda". Kama CUF wakishinda tena uchaguzi utafutwa tena! Huu ndiyo ukweli.
Leo tunamuaga rasmi aliekua rais wa TAnzania Kikwete , na kumkaribisha MAgufuli kama rais kwa miaka mingine 5.
Sisi wazanzibari Tutamkumbuka sana Kikwete , kwa kutunyima haki yetu ya msingi ya kuchagua kiongozi tunaye mtaka.
Tutamkumbuka vyema kwa kusimamia zoezi zima la kuipindua demokrasia Zanzibar kwa nguvu .
tutamkumbuka kwa kufanya hivyo bila ya kujali matokeo na athari ya kuwanyima haki wazanzzibari mbele ya jumuia za kimataifa.
tutamkumbuka kwa kutudhihirishia kuwa huu muungano kwa wazanzibari ni ukoloni , trna ukoloni ule wa kukan damiza hata maendeo ya nchi husika.
anajua wazi kuwa uamuzi wake kulazimisha kuyapindua matakwa ya wazanzibar yatafanya znz kuwekewa vikwazo, yatasababisha nchi kuingia katika ugomvi na nchi kuporomoka kiuchumi.
anajua uhasama wa kisiasa znz utakuwa . Ametumia mamlaka yake kama amiri mkuu wa jeshi kuwa upande wa wanao dhulumu.
ametunyima uhuru wetu wa kuamua . Amekejeli mawazo na maamuzi ya wa znz. Kwa ufupi ametudharau kabisa waznzibar kwa kiwango cha hali ya juu kabisa na kutuonesha kuwa nyinyi hamna lolote na umuhimu wowote kwa tanzania tutafanya tunavotaka tumeku kuhodhini na kuwatawala na hamna haki zozote za kujiamualiwa.
sisi ni wanyonge hatuwezi kupambana na watu million 50 kwa sisi milion moja , ni Mungu peke yake atatulipia na kutulinda na mafisadi wasio penda. kuona wa znz nao wanaishi kwa kujiamulia yale wanayo penda...Allah ni Muweza na ni vyake vyote viliomo kwenye ardhi na mbingu..na yeye ndie mwenye kutoa na kunyima tunamuangukia yeye atupe nguvu ya kutoka katika minyorororo hii ya utumwa na uwaadhiti duniani wote walo finyanga haki zetu na nchi yetu..Amin
tunamtakia heri magufuli na Mungu ambainishie yalokua ya haki.
Nimekusoma na nimefahamu si mfuatiliaji makini wa Siasa za Zanzibar au ni kijana mdogo. Kama utamfikia Mama Samia Suluhu muulize hilo la CCM kutangazwa washindi kwa hisani ya Tume ya uchaguzi na shinikizo la vyombo vya dola. Jambo hilo sio siri.sawa nimekusikiza na nimemsikiza Bi Fatma (Mwanasheria), waswahili wanasema kila mwamba ngozi uvutia kwake. Mimi sidhani na sihafiki kwamba CUF walishinda chaguzi zote zilizopita. CUF itakuwa kichwa cha mamluki kukaa tu kimya na kuna ushahidi wameshindwa chaguzi zote hizo, Maana kama ni kweli, CUF wajiulize swali la msingi, je wao kama chama cha siasa wako hapo kuongoza nchi au kuwa wapinzani, na sidhani jibu litakuwa hilo nalowaza mimi...
Kwangu mimi na watu wote na jumuia ya kimataifa kwa ujumla tunaelewa kwamba CUF hawana support kubwa Zanzibar ndio mana hawakuwa na kura za kutosha kwenye chaguzi zilizopita. kama hilo litabadilika huko mbeleni sijui LAKINI uchaguzi huu umefichua tactics zao za ku-rig uchaguzi huu, HAKUNA mtu kutoka CUF aliyepingwa allegations hizo and so, the allegation will stand, at least for now.
Nafikiri matamko yanabadilika.tayari japo tamko linasema matokeo YOTE yamefutwa,tumeambiwa Yale ya urais Wa Jmt naya ubunge Wa jmt ni safi''Nimeridhika kwamba uchaguzi huu haukiwa wa haki na kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu za uchaguzi," amesema Bw Jecha."Hivyo, kwa uwezo nilionao natangaza rasmi kwamba uchaguzi huu na matokeo yake yote yamefutwa na kwamba kuna haja ya kurudia uchaguzi huu."
Mara hii umesahau mkuu hilo tamko?
Kwa nini uchaguzi urudiwe Zanzibar tu?Kwa Zanzibari tunasubiri siku 90 uchaguzi mwingine ufanywe, kama Maalim Seif alishinda kihalali basi atashinda tena kihalali. tatizo naloliona ni kwamba wanasiasa hawana tatizo na wanacheka pamoja, ila mashabiki wao ndio wanaotaka kuleta matatizo kama Makongoro alivyosema awali.
Nimekusoma na nimefahamu si mfuatiliaji makini wa Siasa za Zanzibar au ni kijana mdogo. Kama utamfikia Mama Samia Suluhu muulize hilo la CCM kutangazwa washindi kwa hisani ya Tume ya uchaguzi na shinikizo la vyombo vya dola. Jambo hilo sio siri.
Kama umemsoma Moyo anataka ushahidi zaidi ya huo?
Angalia video hii dakika ya 2.26 inaipa nguvu makala ya Moyo uliyoisoma.
Kwa nini uchaguzi urudiwe Zanzibar tu?
Uchaguzi urudiwe kwa sheria ipi au katiba ipi?
Kwa nini NEC imemtangaza mshindi wa nafasi ya Uraisi huku kukiwa na utata wa uhalali wa uchaguzi kwa upande wa Zanzibar?
Zaidi ni kwa nini Rais mteule aliapishwa huku kukiwa na utata wa uhalali wa uchaguzi Zanzibar?
Vipindi vya uelimishaji wananchi juu ya kilichotokea Zanzibar na mgongano wa kikatiba na kisheria.
Nimekusoma na naona talking points zako.nimefuatilia sana siasa za Zanzibar, tangu kabla ya kufanya mapinduzi. sidhani kama CUF wana wanawapiga kura wengi. jinsi hali ilivyo ni kwamba uchaguzi itabidi urudiwe. the last election was rigged and marred with corruption, the entire process to that fact was rigged hence there will be another election.
tofauti ya kura za CCM na CHADEMA uraisi ni zaidi ya laki 503,765 hiyo ina maanisha hata Zanzibar wakirudia matokeo ya bara hayata kuwa affected, ndio mana uchaguzi utarudiwa ZNZ tu.
Uchaguzi huu utarudi kwa sheria za Uchaguzi kulingana na Katiba ya SMZ ya mwaka 1984.