Aisee umezaliwa mwaka gani ?Mimi ni Kijana wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 24(Leo ni kumbukizi yangu ya kuzaliwa), pia ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu Bachelor of Science with Education moja ya chuo kikubwa hapa jijini.
Kielimu mimi ni mtu pekee hadi sasa katika ukoo wa baba na mama kufika chuo kikuu, wote kwenye ukoo wa baba na mama walio soma sana wameishia kidato cha nne tena wameambulia four na sifuri.
Wakuu, naandika haya nikiwa na machungu, huzuni na hisia za maumivu makali sana moyoni na akilini mwangu, hasa napotazama familia na yotokea na hali ya uchumi wa familia yangu.
Sina tumaini tena la Maisha, kwa umri wangu huu madogo nimeyaoana maisha ya dhiki na shuruba za Kila namna, nimefanya kazi mbalimbali licha ya kuwa bado na soma Lakini neema ya mafanikio imekataa kabisa kuja upande wangu.
Hapa nilipo natamani japo, nifanye mpango ni ende Africa ya kusini japo kwa kufoji ili nikajaribu bahati yangu, huenda ipo huko, lakini moyo unakata kabisa kufanya maamuzi haya.
Wazazi wangu, siwezi kuwalaumu kwani mimi mwenyewe ni Shahidi wamepambana sana lakini neema na bahati ya mafanikio haijawa upande wao, baba yangu kajaribu Kila aina ya kazi lakini wapi, vilevile mama yangu kafanya bidii sana lakini mambo mabaya.
Nimesoma shule ya msingi hadi advance na badae chuo kikuu, nimesoma kwa tabu sana miaka yangu hiyo, hii ni kutokana na hali ya uchumi wa familia yangu.
Nawaza sana,mwezi mwaka huu namaliza masomo yangu, je kipi kitatokea, wadogo zangu watano Wana- nitazama kaka yao wakiwa na matumaini makubwa sana ndani yao juu Yangu
Stress zinataka kuni maliza, nipo scared sana wakuu
Barikiwa sana aiseeNimekupenda bure walayi
Asante aisee,nipatie baraka ya ndani🤣🤣Barikiwa sana aisee
🤣🤣🙌🏿Asante aisee,nipatie baraka ya ndani🤣🤣
Acha upumbavu wewe kijana mdogo. Kwanza kinachokupa stress ni nini wakati hata hayo maisha hujaanza? Kama uko chuo soma kwa bidii furahia uanafunzi wako. Ukiendelea na huu upumbavu wa kujipa stress za kishamba utaishia pabaya.Nawaza sana,mwezi mwaka huu namaliza masomo yangu, je kipi kitatokea, wadogo zangu watano Wana- nitazama kaka yao wakiwa na matumaini makubwa sana ndani yao juu Yangu
Stress zinataka kuni maliza, nipo scared sana wakuu
Alafu unaonekana pisi kali fulani ivi😀😀🤣🤣🙌🏿
Haya bhana🙏🏽👋Alafu unaonekana pisi kali fulani ivi😀😀
Huyo hata kuajiriwa hafai ataenda kufundisha stress watoto wetu tu mashuleni.Mheshimiwa Dr Samia Suluhu Hassan mama yetu....tunajua uliachiwa mzigo mkubwa wa mlundikano wa wasioajiriwa lakini tunaomba mama,jitahidi hivyohivyo uajiri vijana....jamani hali ni mbaya huku mtaani....vijana ambao ndiyo nguvu ya taifa Wamekosa matumaini ya nchi na kuishi
He is too young to complain unless hana akiliMkuu,Ushauri wangu kwako ni huu,Stop Thinking and Start Doing.Wewe ni mpambanaji na ni Mshindi.Mungu yuko Upande wako.
Ningekuwa mimi ndiyo wewe, nisingelia usiku kucha kwa sababu kama hizi ulizozitoa hapa!Mimi ni Kijana wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 24(Leo ni kumbukizi yangu ya kuzaliwa), pia ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu Bachelor of Science with Education moja ya chuo kikubwa hapa jijini.
Kielimu mimi ni mtu pekee hadi sasa katika ukoo wa baba na mama kufika chuo kikuu, wote kwenye ukoo wa baba na mama walio soma sana wameishia kidato cha nne tena wameambulia four na sifuri.
Wakuu, naandika haya nikiwa na machungu, huzuni na hisia za maumivu makali sana moyoni na akilini mwangu, hasa napotazama familia na yotokea na hali ya uchumi wa familia yangu.
Sina tumaini tena la Maisha, kwa umri wangu huu madogo nimeyaoana maisha ya dhiki na shuruba za Kila namna, nimefanya kazi mbalimbali licha ya kuwa bado na soma Lakini neema ya mafanikio imekataa kabisa kuja upande wangu.
Hapa nilipo natamani japo, nifanye mpango ni ende Africa ya kusini japo kwa kufoji ili nikajaribu bahati yangu, huenda ipo huko, lakini moyo unakata kabisa kufanya maamuzi haya.
Wazazi wangu, siwezi kuwalaumu kwani mimi mwenyewe ni Shahidi wamepambana sana lakini neema na bahati ya mafanikio haijawa upande wao, baba yangu kajaribu Kila aina ya kazi lakini wapi, vilevile mama yangu kafanya bidii sana lakini mambo mabaya.
Nimesoma shule ya msingi hadi advance na badae chuo kikuu, nimesoma kwa tabu sana miaka yangu hiyo, hii ni kutokana na hali ya uchumi wa familia yangu.
Nawaza sana,mwezi mwaka huu namaliza masomo yangu, je kipi kitatokea, wadogo zangu watano Wana- nitazama kaka yao wakiwa na matumaini makubwa sana ndani yao juu Yangu
Stress zinataka kuni maliza, nipo scared sana wakuu
Kimsingi hali ya maisha mtaani ni tete.Hizi mada za vijana kuwa depressed mbona zimezidi sana humu jukwaani! Hili ni tatizo.