Niliyoyashuhudia Jeshini

Haha mimi nililenga mijusi mkuu wapo wale masniper wenyewe walioweza, intake yetu waliolenga nyingi sana ni tatu hakuna aliyepata zote tano, hapo kwenye kudoji umenikumbusha kuna afande alikuwaga anasema kuruta nikikukuta umedoji uwe peke yako nitakuacha ila mkiwa wengi andaeni nguvu tu
 
Tofauti ni Nini?
jkt ni wasimamiaji miradi ya ujenzi wa Taifa ni nadra sana wao kuwakuta wanaenda mission... kama hao unao sikia wameenda congo central Africa na kwengineko...

wengi huwa ni watu wenye fani mbali mbali za ujenzi, kilimo, ufugaji...huwa wanapata mafunzo kidogo ya ukakamavu...ila kozi zao huwa ni kwaajili ya uzalishaji mali ana ufundi...!

jwtz ndio hao unao waona au kusikia kuwa wameenda mission mbali mbali congo huko...kwenye maswala peace making...

ulinzi wa nchi kwa ujumla na mipaka upo mikononi mwao kwa ujumla. hawa kozi zao huwa ni za utambuzi wa magaidi na maadui wa nchi {sio vibaka au wezi🤣🤣🤣}na jinsi ya kupambana nao. iwe ndani ya mipaka au nje ya mipaka.

jwtz wanajifunza mambo ya kivita na silaha zote za kivita...ila jkt hawana mambo hayo...!​
 
Hv wale wa Ruvu Prince Mhando Jadda D Metakelfin mlishawahi pangwa kule bwawa la samaki
Huko sijawahi pangwa mkuu yani kwa kifupi kitengo cha mifugo sijawahi kuwa na zali nacho ni siku moja tu nilipangwa kule poultry kuokota mayai ya kuku basi, mimi shamba langu lilikuwa kule jkt club karibu na barabara ya kwenda mikoani, tulikuwaga tunanunua vitafunwa kule kule mtu unarudi kikosini ushashiba zako
 
Hv wale wa Ruvu Prince Mhando Jadda D Metakelfin mlishawahi pangwa kule bwawa la samaki
mimi niliishia kwa kuku🤣 na ng'ombe...kwa ng'ombe nilikuwa naweza kumnyonya ng'ombe kama ndama...harafu siku kaa sana hapo...

tulipigwa kibogo cha kwenda dodoma kwenye dhabibu kisha oljoro...nikamaliza muda nikarudi uraiani...

hivi sasa naendesha tu boda boda yangu jiji la darisalama...wenzangu wananishangaa jinsi ninavyo kamatwa na trafick na kuachiwa muda huo huo bila kutoa chochote🤣🤣🤣

jeshi limeniwekea kinga kubwa sana ya kukamatwa 🤣🤣🤣 kwa kifupi sijawahi kukamatwa na haitatokea nikamatwe​
 
Mwendo mgumu huo
Ulinifanyaga nikatimuliwa special group na afande tall - kANA -
 
Hio ni oljoro kutoka dar hadi Arusha ni masaa 8 9,akishuka stand achukue bajaji za kuwapeleka kilombero stand akapande hiace za oljoro​
baridi la oljoro asingeliweza mtoto wa mama huyu...huyu hajavika Tanga amini nakwambia...pale mrombo hiace zinaenda moja kwa moja hadi oljoro labda kama siku hizi kuna bajaji....!

kulikuwa kuna hiace ambazo ikifika jioni hujapanda uwakika wa kwenda kwa mguu hadi oljoro ulikuwa mkubwa sana🤣🤣🤣​
 
Oljoro wanapitia mrombo/ Njiro- atomic?
 
umecopy na kupast hayo maneno hayatumiki siku hizi...🤣🤣🤣
Tatizo lako utoto unakupa shida.
Hivi umeona kuna sentence imeambatana na hayo maneno? Kwa kuwa umepita JKT basi umekuwa mmiliki wa misemo ya jeshini sio? Kuna sehemu mtoa mada kasema tu comment mambo ya siku hizi? Pole sana dogo ujuaji utakuponza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…