si ugonjwa ndugu..ni uzembe na uvivu katika kujiangalia na kufuata kanuni za afya!
Usafi wa mwili hasa kwa wenzetu akina kaka si kitu kinapewa sana kipaumbele ( naomba radhi kwa wale wasiohusika - wale wenye kujijali msije mkanirarua ilahali haiwalengi wote).Wengi hawajali kunyoa makwapani na kwingineko, kujisugua wakati wa kuoga, kutumia maji ya moto/uvuguvugu kwa kupata matokeo mazuri ya usafi, kutumia muda wa kutosha bafuni - mtu anaingia sha-shaa keshatoka eti kaoga!
Kushindwa kutumia muda wa kutosha , ndipo hupelekea kuacha shombo na kuendelea kuzalisha bacteria kwa kasi juu ya ngozi.Hili huleta harufu.kINGINE NI kutokubadili nguo hasa za ndani baada ya kuoga.Utaachaje kunuka?
Kazi za makonda na madereva kutwa kukaa kwenye mavumbi, joto na jasho hutoka kwa wingi na kukaukia... kama haogi usitegemee hali tofauti.