Aisee umeongea maneno ya busara sana. Lakini nmeangali clip, ni fupi lakini nadiriki kusema Mh HAKUSEMA hayo tuliyafikiria na kuyajadili. Hata hivyo, mjadala huu umesaidia kwa kiwango kikubwa viongoz wetu wajue Watanzania wanafuatilia ustawi wa nvhi yao. Kauli yoyote tatanishi itazua mjadala tu.Kauli ya Ndalichako(kama kweli alisema hivyo) ya kwamba mwenye sifa ya kuingia chuo kikuu ni form six leaver tu, tena aliyefaulu, inavunja katiba ya nchi, sheria ya elimu ya mwaka 1978, Haki za binadamu, sheria za kimataifa(International laws) ambazo TZ ni mwanachama, Sera ya Elimu ya mwaka 2014, Ilani ya CCM(2015-2020), na miongozo mbalimbali ya elimu nchini. Mimi na mwana CCM hai. Napingana kabisa na kauli hiyo, kwasababu inawanyima haki watoto wa masikini wanaosoma shule za kata kupata haki ya kusoma chuo kikuu. Ata re-sit form 6 hadi lini? Kwa gharama ya nani? "Justice delayed is justice denied." Tuangalie hali halisi na tuwe wakweli. Huku vijijini ktk shule za kata walimu wachache, maabara hakuna, vitabu hakuna, umeme hakuna, maji shida, matibabu duni, pesa kwaajili ya ada na michango mbalimbali shida, matatizo mengi ya kifamilia kwasababu ya umasikini, nk. Hivyo ni vigumu sana vijana kufanya vizuri ktk mitahani yao. Sisi watu maskini equivalent qualification ya kuingia chuo kikuu ambayo ni diploma imetusaidia sana kuingia chuo kikuu. Tunapomaliza form 4 au 6 kama tumefeli, huanza kusomea taaluma ya "kazi" kwa kiwango cha certificate au diploma ili tujiendeleze huku tukiwa kazini. Kwahiyo, kauli yake hiyo imetoka kwenye kinywa cha "tajiri" anayeishi Masaki, asiyejua kuwa kuna masikini wengi ktk nchi hii, hasa vijiji. Hiyo kauli ikiachwa itekelezwe, itakuwa vigumu sana kwa sisi masikini kusoma vyuo vikuu. Vyuo vikuu vitakuwa kwaajili ya watoto wa matajiri tu. Na ikiwa hivyo masikini tutaenda kuipinga mahakamani. Tunapotoa kauli mbalimbali(executive orders) tuangalie hali halisi na haki za walio wengi, hasa masikini. Kifanyike nini: 1.TCU/NACTE kuweka cut-off GPA ya mwenye diploma kuingia chuo kikuu.
2.NACTE/TCU kufuatilia ubora wa utoaji elimu ktk vyuo vya kati na vyuo vikuu.
3. Vyuo vinavyotoa elimu ya kati visipandishwe hovyo kuwa vyuo vikuu. 4.Maamuzi/matamko mbalimbali,hasa yanayogusa haki na masilahi ya wengi yasitamkwe kwa mihemuko ya mtu moja(abuse of discretionaly powers),bali yawe ni tunda la maamuzi ya wengi/shirikishi(wadau, wataalamu na kamati mbalimbali ambazo zipo kisheria).
5.Uhuru wa mtu kuamua afikie malengo yake kwa njia ipi, ulindwe. 6.Kabla ya kutoa matamko tusome katiba ya nchi, sheria na sera mbalimbali ambazo zinagusa jambo hilo(Rule of Law).
7.Kutaka sifa na kujenga majina yetu mbele ya wateuzi, kusiwe chanzo cha kunyang'anya haki za masikini ambao hawana uwezo wa kujitetea.
Note: Ni kweli tunahitaji kuboresha elimu, lakini ktk kufanya hivyo tuzingatie katiba ya nchi, sheria ya elimu, sera ya elimu, maamuzi shirikisha, ilani/manifesto, kufanya tafiti kabla ya kutoa tamko.
Man una talk as if diploma is for free... nenda vyuo vya ufundi man.. diploma kuipata ni ume hustle. Alaf si wote wanaosoma diploma wamefeli... wengine walifaulu form 4 tena div 2 lakin hawakutaka kwenda advanced..Mi naona mama yuko sawa haiwezekani mtu ana D NNE yaani div 4 mbovu.....aunge unge cert aje Diploma halafu apate degree,,huku kidato cha NNE alipata alama mbovuuu.....
Umekariri brother.... embu nenda dit... kacheki diploma zao zilivyo... alaf ndio urudi hapaMi nachojua diploma ngumu ni ya ualimu tu...hizo zingine mnapewaga tu.....
Bhasi tuache kuchukua 4 mbovu kujiunga na Certificate
Ha ha ha ha [emoji40] [emoji40] [emoji40]Acheni unafiki nyie sindiyo mlikuwa mnakesha JF kumuomba rais Magufuli amchague kuwa waziri.
Sisi tunamjua siku nyingi tuliwambia kuwa huyu dada ana matatizo mlitushambulia sana.
Tulieni sasa mnalia lia nini.
Miaka niliyosoma mimi walikuwa wanaondolewa karibu wote 1st year kwaku disco . . . . Yaani akikatiza physical chemistry , statistics na engineering ujue lazima alipitaga A level otherwise utaona tu rangi nyekundu . Sijui siku hiziUnataka kuniambia huko diploma huwa hawafanyi mitihani ya kuchujwa na wasiofaa kutupwa nje??
Hebu kama una mtoto anaesoma au aliyekwisha kusoma chuo muulize kuhusu hao watu waliotokea diploma huwa wanakuwa vipi darasani?
Kwa taarifa yako MTU anaweza toka darasa LA saba hadi pale mwisho unapopajua wewe kielimu na akawa bright,tens hao waliowengi wanakuaga vichwa mpaka unashangaa,alafu mabadiliko ya elimu hayafanywi haraka HVO ni mfumo ubaobadika kidogo kidogo kwa awamu,huwezi amka tu asubuhi ukaja na mabaduliko yako,unahitaji kuwajuza watu mbalimbali wadau katika elimu,mabadiko kila kukicha wakati huo huo mazingira wezeshi ni yaleyale,hakuna maabara,vitabu,walimu wachache na walioko bado sana malalamiko yao,mfano kubasilisha tu GPA ilitakiwa ichukue hata miaka miwili na kuwafanya wale waliokuwa wanasoma kipindi cha GPA kabla haijabadilishwa wamalize kabisa then wanaojiunga nyuma yao ndio wakumbane na hayo mabadiliko,sasa huyu mama toka ameingia mabadiliko yaliyotokea hata kumi yanafika just kwa mwaka mmoja tuu,hata madogo wanafaulu hata chuo hawaingii,waliomaliza darasa ma saba wengi wamekosa nafasi,sasa sijui lengo lake ni nini? Mara mia hata Mungai au murugo sio huyu mamaMi naona mama yuko sawa haiwezekani mtu ana D NNE yaani div 4 mbovu.....aunge unge cert aje Diploma halafu apate degree,,huku kidato cha NNE alipata alama mbovuuu.....
wenye elimu ya kuunga unga siyo maskini acha kusingizia maskini.Kauli ya Ndalichako(kama kweli alisema hivyo) ya kwamba mwenye sifa ya kuingia chuo kikuu ni form six leaver tu, tena aliyefaulu, inavunja katiba ya nchi, sheria ya elimu ya mwaka 1978, Haki za binadamu, sheria za kimataifa(International laws) ambazo TZ ni mwanachama, Sera ya Elimu ya mwaka 2014, Ilani ya CCM(2015-2020), na miongozo mbalimbali ya elimu nchini.
Mimi na mwana CCM hai. Napingana kabisa na kauli hiyo, kwasababu inawanyima haki watoto wa masikini wanaosoma shule za kata kupata haki ya kusoma chuo kikuu. Je kijana huyu ata re-sit form 6 hadi lini? Kwa gharama ya nani? "Justice delayed is justice denied".
Tuangalie hali halisi na tuwe wakweli. Huku vijijini ktk shule za kata walimu wachache, maabara hakuna, vitabu hakuna, umeme hakuna, maji shida, matibabu duni, pesa kwaajili ya ada na michango mbalimbali shida, matatizo mengi ya kifamilia kwasababu ya umasikini, nk.
Hivyo ni vigumu sana vijana kufanya vizuri ktk mitahani yao. Sisi watu maskini equivalent qualification ya kuingia chuo kikuu ambayo ni diploma imetusaidia sana kuingia chuo kikuu.
Tunapomaliza form 4 au 6 kama tumefeli, huanza kusomea taaluma ya "kazi" kwa kiwango cha certificate au diploma ili tujiendeleze huku tukiwa kazini.
Kwahiyo, kauli yake hiyo imetoka kwenye kinywa cha "tajiri" anayeishi Masaki, asiyejua kuwa kuna masikini wengi ktk nchi hii, hasa vijiji.
Hiyo kauli ikiachwa itekelezwe, itakuwa vigumu sana kwa sisi masikini kusoma vyuo vikuu. Vyuo vikuu vitakuwa kwaajili ya watoto wa matajiri tu.
Na ikiwa hivyo masikini tutaenda kuipinga mahakamani. Tunapotoa kauli mbalimbali(executive orders) tuangalie hali halisi na haki za walio wengi, hasa masikini.
Kifanyike nini:
1. TCU/NACTE kuweka cut-off GPA ya mwenye diploma kuingia chuo kikuu.
2. NACTE/TCU kufuatilia ubora wa utoaji elimu ktk vyuo vya kati na vyuo vikuu.
3. Vyuo vinavyotoa elimu ya kati visipandishwe hovyo kuwa vyuo vikuu. Vyuo vya kati ni msaada mkubwa sana kwa vijana, hasa maskini vijijini.
4. Maamuzi/matamko mbalimbali,hasa yanayogusa haki na masilahi ya wengi yasitamkwe kwa mihemuko ya mtu moja(abuse of discretionaly powers),bali yawe ni tunda la maamuzi ya wengi/shirikishi(wadau, wataalamu na kamati mbalimbali ambazo zipo kisheria).
5. Uhuru wa mtu kuamua afikie malengo yake kwa njia ipi, ulindwe.
6. Kabla ya kutoa matamko tusome katiba ya nchi, sheria na sera mbalimbali ambazo zinagusa jambo hilo(Rule of Law).
7. Kutaka sifa na kujenga majina yetu mbele ya wateuzi, kusiwe chanzo cha kunyang'anya haki za masikini ambao hawana uwezo wa kujitetea.
Note: Ni kweli tunahitaji kuboresha elimu, lakini ktk kufanya hivyo tuzingatie katiba ya nchi, sheria ya elimu, sera ya elimu, maamuzi shirikisha, ilani/manifesto, kufanya tafiti kabla ya kutoa tamko.
Hata ukiwa kazini na una cheti au diploma unaweza kusoma five &six hatimae ukapata vigezo vya kusoma digrii. Watanzania wenzangu tupunguze kulalamika kwa kila kitu, nani alikwambia maskini hawezi kifaulu? Wasomi asilimia kubwa vyuoni wamesoma shule za kata.
Fallacy of generalization. It is your misconception. Nimemaliza Form 6, tena PCB. Sijawahi unga hata siku moja. Lakini any reasoble and fair minded person lazima aangalie na kuzingatia haki za wengi, hasa wanyonge(voice of the voiceless).I am of that calibre.
wewe una unafiq mpaka basi, wewe unajua mazingira ya kupata form four dddd? kuna watu wakiletwa dar wakapata tuishen wanapasua, mtu anatoka vijijini alikuwa na akili lakini wakampeleka shule za kata walimu hakuna unategemea nini?Mi naona mama yuko sawa haiwezekani mtu ana D NNE yaani div 4 mbovu.....aunge unge cert aje Diploma halafu apate degree,,huku kidato cha NNE alipata alama mbovuuu.....