Nauza Eneo la Heka Moja Mlandizi

Nauza Eneo la Heka Moja Mlandizi

Bei: Tsh 3,000,000
Ukubwa: Hekari Moja (70m X 70m) eneo ni tambarare kabisa..
Lipo kijiji cha Kikongo 7km kutoka Mlandizi mjini (Barabara ya Morogoro), 57km kutoka Ubungo.
Lipo karibu na Barabara ya kuelekea Stesheni ya Mzenga ambayo inajengwa kwa kiwango cha lami.
Barabara ya kuingia shambani ipo, hivyo unafika mpaka shambani kwa gari.
Lipo karibu na eneo la makazi ya watu, jirani kuna shule na Pia Zahanati ya Kijiji.
Lipo karibu sana na Bomba la maji la kijiji. Pia Umeme upo Mita chache kutoka shambani.
Linafaa kwa Kilimo, Makazi, kujenga Godown, Hoteli, Mabanda ya Mifugo n.k
Udongo ni mzuri na nimewahi kuotesha humo mihogo, limeshasafishwa na kung'olewa visiki.
Mazao yanayostawi: Mahindi, Mihogo, Mananasi, Mapesheni, Mbaazi, Mikorosho n.k
Pia jirani kuna mradi wa Bwawa la samaki, Shamba la maembe ya muda mfupi, na Michungwa.
Pia jirani kuna shughuli za ufugaji wa mifugo kama kuku, Nguruwe n.k.
Pana usalama wa kutosha kwa mali zako.
Lina miti kadhaa ya Mikorosho.
Sipendi kuliuza ila ni kwa vile tu nakosa muda wa kulisimamia, hivyo nataka nielekeze nguvu kwenye shughuli ninazofanya sasa..


Simu: 0688 382 415
Mimi ndiye mmiliki halali na vibali vya umiliki nitakupatia kwa mujibu wa sheria na taratibu za Serikali ya Kijiji.

Bei yake?
 
Kwanini shamba lako umekuwa ukitafuta mteja kwa mwaka wa pili sasa na haupati mteja? lipo sehemu mbaya? halina vibali? kuna lolote lile unalodhani yaweza kuwa ni sababu? Nimeuliza hivyo kwakuwa, mwaka 2013 ulipost tangazo hilo hilo, hili hapa https://www.jamiiforums.com/matangazo-madogo/568946-shamba-hekari-moja-linauzwa-mlandizi.html
mwaka 2013 huo huo ulipost tangazo hilo hilo, hili hapa https://www.jamiiforums.com/matangazo-madogo/567739-shamba-hekari-moja-linauzwa-mlandizi.html

Posted by: SUPU YA MAWE
 
Last edited by a moderator:
na hata hili tangazo nimekopi tu tangazo la kipindi kile kisha nikabadili tu bei..

lipo sehemu nzuri na ni tambarare.

halina mgogoro na kama utahutaji kuliona na uko dar nijulishe nikupeleke wikiend hii, gharama juu yangu maana nina mpango wa kwenda kupacheki kesho au keshokutwa.

Bro nahitaji km vipi ni pm ili nikapaone w.nd hii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom