Nauliza tu

Hapana, hapafai hapo. Si halali
 
anachukia ndugu wote au baadhi? Kuna ndugu wengne ni shida sana usipokuwa makini wanaweza kukuharibia ndoa wana chokochoko hadi basi. We chunguza kwa busara zako uone nani chanzo kama ni mke wako mshauri katika minajili ya kumbadili hiyo tabia na kama ni ndugu zako washauri pia katika mantiki ileile. Mnarekebishana mnaendelea kuishi na mkeo ndoa ni ya thamani sana
 
Kuna ndugu wengine wagumu... na mama wakwe wengine mweeeeee.... ni sheeeeda! Ila mwanamke mwerevu anaungulia moyoni nje anacheka tu... kama vipi analilia bafuni akiwa anaoga! Kilio cha samaki machozi yanaenda na maji...
 
Hawapendi kivipi...anawatukana, ananuna wakiwatembelea, anatamka kabisa siwapendi, au?

Tafuta kiini...

Je ameanza lini kuwachukia? Umemuuliza sababu?
Ukimuacha una mpango wa kuoa tena? Unamuoa nani? na unajisikiaje kufanya maamuzi makubwa kama hayo - divorce? Bado unampenda au umepata sababu ya ziada (kuchukia wazazi) ya kumuacha?
 
Kuna ndugu wengine wagumu... na mama wakwe wengine mweeeeee.... ni sheeeeda! Ila mwanamke mwerevu anaungulia moyoni nje anacheka tu... kama vipi analilia bafuni akiwa anaoga! Kilio cha samaki machozi yanaenda na maji...
Umeanza kunivutia hivyo, halafu nikivutika unambwela!!!!
 
Daa wanawake bwana,shemeji alikuwa anaelewana sn na mama lakini alipofariki kaka heeeeeee makucha yote nje.Inauma sn,wakati anapigania kuolewa mama ndo alikuwa kimbilio.
 
Kuishi kimasikini ni kuishi nyumba moja mkeo na dada,zako na mama yako....utampa mkeo lawama za bure...kila mwanamke anataka kuwa na sauti nyumbani kwake...sio kuishi kinyonge...

Nin sababu inayopelekea uishi wew na mkeo nyumban kwenu??? yan kuna dada mama wadogo zako........ nin sababu???
 
Haleluiya

Mleta mada anyooshe maelezo

usikute nyumba yake inarndeshwa na ndugu zake halafu anategemea mkewe awe na upendo utatoka wapi?

Aeleze ndugu zake wanaishi wapi
Anaoishi nao wangapi
Maanuzi ya nyumbani kwake anafanya nani
Tabia za ndugu zake zikoje
Tabia ya mkewe ikoje
Kwa nini anadhani mkewe hawapendi ndugu zake etc etc


Kuishi kimasikini ni kuishi nyumba moja mkeo na dada,zako na mama yako....utampa mkeo lawama za bure...kila mwanamke anataka kuwa na sauti nyumbani kwake...sio kuishi kinyonge...
 
Kuishi kimasikini ni kuishi nyumba moja mkeo na dada,zako na mama yako....utampa mkeo lawama za bure...kila mwanamke anataka kuwa na sauti nyumbani kwake...sio kuishi kinyonge...
Umasikini ni tatizo mkuu....
Hata tukipata hela ukubwani bado ni tatizo kwani tulilelewa kwenye umasikini ,muda wote ni mapambano tu ya kujilinganisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…