Natafuta mchumba

JCTR

Member
Joined
Oct 23, 2016
Posts
13
Reaction score
10
Mimi ni kijana wa kiume, nina miaka 30. Nimehitimu elimu ya Chuo Kikuu ngazi ya Uzamili. Kazi ni Mhadhiri na ninaishi Mwanza.

Wana JF, natafuta mchumba mwenye umri usiozidi miaka 30 na isiyopungua miaka 24. Dini, rangi, kabila na elimu sibagui ila awe mwenye tabia njema na akiwa ameshajifungua basi wasizidi watoto watatu.

Mimi napenda sana kuangalia muvi, kusoma vitabu, kupiga kinanda na kuimba (Ingawaje sina kipaji), pia napenda sana kusaidia watu wasiojiweza hasa yatima na wajane. Wakuu, udhaifu wangu mkubwa ni kunywa sana pombe ingawaje sivuti sigara.

Kwa hayo machache, naomba kwa mwanamke yeyote ambaye kwa kuzingatia nilichosema, anajua yuko tayari kuwa nami basi tuwasiliane privately.

NB: SIJAOA WALA KUWA NA MCHUMBA MPAKA LEO KWA SABABU YA MAISHA TU.

Nawasilisha.
 
Kusanya zako hela mkuu..jenga li ghetto lako nunua li usafir la ukweli kama ni kiu tafuta ya kupiga ipite hiv
.
hawa wanawakee wanateesa akili,tena hawa wa kutafuta online achana nao kabisa.Nina umri kama wako kwa sasa nimeshapitia mengi in short najuta sababu nimerudishwa nyuma kimaendeleo.
 
Ni kweli Mkuu ila naamini inawezekana pia kupata huku online. Shuhuda za watu waliopata wenzi online ziko nyingi tu,jambo la msingi ni kuwa makini.Nakuomba usikate tamaa Mkuu,popote waweza pata mwenzi iwe kanisani,msikitini,barabarani,ufukweni nk.
 
Hongera kwa maamuz ya kutafuta mchumba na kuwa atakuwa mke wako , bt mm nakushaur kuwa cc wana jf hatuwez kujua yp mke bora au xo bora .M m naomba umushirikishe Mungu kwanza yy ndy atakuonyesha yp wa kkfaa .
 
Hongera kwa maamuz ya kutafuta mchumba na kuwa atakuwa mke wako , bt mm nakushaur kuwa cc wana jf hatuwez kujua yp mke bora au xo bora .M m naomba umushirikishe Mungu kwanza yy ndy atakuonyesha yp wa kkfaa .
Asante sana,umenena kweli kabisa
 
Mkuu kwenye hiyo hadhara unayohadhiri hujapata bint wa kuoa?

au hadhara yako ni ya wanaume tupu?
 
Ni hadhara mchanganyiko- Wanaume na Wanawake. Sijapata Mkuu
Jipinde mkuu umpate shemeji kutoka hapo kwenye hiyo hadhara kwani waliomo humu JF ni hawahawa tunaowaona katika ''shughuli zetu'' za kila siku.
 
Jipinde mkuu umpate shemeji kutoka hapo kwenye hiyo hadhara kwani waliomo humu JF ni hawahawa tunaowaona katika ''shughuli zetu'' za kila siku.
Nashukuru sana kwa ushauri Mkuu ingawaje nadhani ni busara zaidi kama nisipojifunga kwamba ni lazima nipate kwenye hiyo hadhara tu!Minadhani ni vyema zaidi kuwa na uwanja mpana zaidi ili niweze kupata ambaye atakuwa bora zaidi-Ndio sababu na humu JF nimeamua kutupa karata Mkuu
 
Mkuu kama umesoma vizur nilichokiandika,utakuwa umegundua kwamba sikujielekeza kabisa katika mwonekano wa kimwili, hivyo hukuwa na sababu ya kunitumia picha na kuniuliza,ulichotakiwa kufanya ni kuniunganisha nae tu Mkuu
Hahaha wewe jamaa unanichekesha sana kwanza kwa hivyo vigezo eti kama ana watoto wasizidi watatu ...jamaa hapa kakupa picha unashangaa kwanini haja kuunganisha badala ya maneno mengi ....

Unatafuta mke au mtu wa kumtoa kafara ?
 
Hahaha wewe jamaa unanichekesha sana kwanza kwa hivyo vigezo eti kama ana watoto wasizidi watatu ...jamaa hapa kakupa picha unashangaa kwanini haja kuunganisha badala ya maneno mengi ....

Unatafuta mke au mtu wa kumtoa kafara ?
Kigezo cha watoto watatu ni kwa sababu mimi binafsi sioni na wala sijawahi kuona kama watoto wa mwanamke ni tatizo (Ndio maana kuna watoto kadhaa ambao nawalea kama wangu na nikijaliwa uwezo nitaongeza - Sasa kwa nini nimetaja wasizidi watoto hiyo ni kwa sababu ndo napenda iwe hivyo sasa kwa nini napenda hivyo hapo kwa kweli sijui Mkuu )

Hoja ya kumtoa kafara nayo haupo Mkuu, nimesema wazi kuwa natafuta mchumba ili panapo majaaliwa awe mke. Mkuu, kwa hakika,sijagusia kabisa swala kwamba nataka mwanamke ili nimtoe kafara
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…