Natafakari siku Job Ndugai atakapojiunga na CHADEMA mapokezi yatakuwaje pale Ufipa!!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,124
142,214
Katika siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu.

2020 wagombea wa CCM wengi watakaokatwa mikia watapenda kupitia daraja la Chadema kuingia bungeni kama ilivyokuwa 2015 na baadae wataunga mkono juhudi kama ilivyofanyika 2018.

Endapo mh Ndugai atajiunga na Chadema ili kugombea nafasi kubwa zaidi sipati picha jinsi makamanda watakavyowageuka CAG na Masele plus yule Nassari na kummwagia misifa lukuki spika mstaafu wakati huo.

Natafakari tu
Maendeleo hayana chama!
 
Yaelekea wewe huwa husomi vitu vya sasa. Chama chrtu pendwa kimepitisha sheria MTU kuhamia Chama ruksa lkn kugombea ni lazima uwe mwanachama wa Chama husika kwa zaidi ya miaka 2. Hapo. Waliwakomoa wenzao kumbe wanajikomoa. Wapatapata tabu sana
 
Ndugai hatapokelewa na chama chochote cha upinzani,hana sifa za kuwa mpinzani
 
Sidhani chadema watarudia kosa walilolifanya. Huoni hata sumaye wameshamzima, hasikiki sana siku hizi.

Ndugai ni liability, Makapi ni liability.
 
Umesahau kumalizia kua ccm ni mama wa ANC Afrika Kusini
 
Itakuwa ni shangwe na vigelegele. Makamanda watakwenda mbali zaidi na kusema sasa wamelipata jembe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…