Naombeni ushauri

Mr General

Member
Joined
Mar 26, 2014
Posts
22
Reaction score
1
Nimekuwa katika mahusiano na binti mmoja.Tumekaa nae kama miaka 4 bila kufanya nae tendo la ndoa kipindi hicho bado tunasoma.Baadhi ya marafiki wanasema kuwa ana HIV.Lakini naogopa kumwambia wasemavyo.Na yeye bado ananipenda.Nami nilishahamisha mawazo kwake.Nifanye je?
 

mimi naweza kukuambia kuwa usiwape watu nafasi ya kuingilia sana mapenzi yako.USHAURI...wewe mwambie mpnz wako kuwa mkapime kwa mapenzi yote na sio kama njia ya kuepusha shari,then mkishapata majibu ndo utajua mbivu na mbichi kwani HAUWEZI KUMUACHA MPENZI WAKO KISA MANENO YA WATU..kila la kheri.
 
Hiv wewe unauliza nini sasa?si umchukue mkapime??unaemuoa ni huyo dada au ni hao watu wanaokuletea maneno?
 
Mr. general miaka 4?? inaonekana tayari umeshamtafuna sana tu, kwhyo unachotaka tukutoe wasi wasi, kwanini msiende kupima wote ili upate uhakika, si unajua binadamu wamezaliwa wanasema, na vp ulishapata marafiki kwenye uzi wako ule??
 
pigeni shule nyie, acheni kuambukizana ngoma
 
Fanya atafiti, utaujua ukweli, usipende sikiliza ya watu sana bila ya kuchunguza.
 
Kwenda kupima ndo solution

Halafu kwa nini unasikiliza maneno ya watu???

Ila kama haunz hisia nae muache kwa amani


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Lisemwalo lipo kama halipo linakuja! Chukua hatua nenden tu mkapime ndo muanze shughul za kugegedana
 
Nyie watoto mtatutoa roho, mapenzi shuleni siku hizi ni hatari sana.
Watoto wachache sana wa shule wanaweza fanya maamuzi ya kupima.

Lakini haiondoi kuwa kuna watoto wanaozaliwa na VVU na kukua na kuishi na VVU, kama hawakufundishwa kuwalinda wenzao, basi nao wanajiachia tu, kama ujuavyo ujana maji ya moto.

Kuna mtoto namfahamu, kawaammbukiza sana wenzie bila kujua na baada ya kujua. Kwao hawakumwambia kamaa ni mwathirika hadi alipomaliza F4, tena ni baada ya CD4 kuanza kushuka na kuugua. Madaktari walishauri aambiwe sababu ngono inamfanya awe weak zaidi, je alikuwa keshaambukiza wangapi?

Hata baada ya kwenda high skul aliendelea kuwagegeda tu.

We kijana, kama mzazi nakuushauri uachane na ngono kwa sasa, ila kama kweli mnapendana nendeni mkapime. AIDS is real.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…