The Hidden
JF-Expert Member
- Mar 26, 2017
- 246
- 101
Tangu niwe na mpenzi wangu ni miaka miwili sasa imekatika, tumekuwa tukigombana mara kadhaa na mengine makubwa zaidi ya hili lilotokea sasa, yaani ilikuwa juzi nilipokutana na msala fulani kazini na nikamwambia huyo mpenzi wangu kwamba nilitegemea kwa msala ule mdada ninayefanyanaye kazi ofisi moja angenisaidia kwasababu tulifahamiana zamani sana kabla ya kukutana hapo kazini tena lakini nashangaa ndiye aliyenikandamiza kabisa.
Huyu mpenzi wangu anawivu sana, kitendo cha kumwambia hivyo tu alipanic na mimi nikamwambia "huo wivu ni wa kipuuzi" kusikia hivyo akapanic zaidi na kukata simu, baada ya hapo nilimchunia kidogo kwa siku tu japo si kawaida yangu, baada ya hapo.
Nikamtafuta kwa simu kwa sababu sasa tuko mbali kikazi(mikoa tofauti ) lakini hakupokea simu ila akatuma SMS kwamba"siku nzima umenisahau sababu ya huyo mdada ndo unanitafuta sasa, sihitaji simu yako " baada ya hapo nilipiga simu sana hakupokea mpaka hapo jana alipopokea na kusema haitaji mahusiano tena na haitaji tena kuolewa ila tubaki marafiki tu huku akikumbushia mambo mazito sana nilomkosea huko nyuma lakini kwa mbinde tukarudiana.
Wakuu, kauli yake imenichanganya na anaonekana hajali. Naombeni ushauri wenu sababu bado nampenda, na hata yeye tukiwa katika amani alionesha kila dalili za upendo lakini anaonekana ni mtu mwenye maamuzi magumu.
Huyu mpenzi wangu anawivu sana, kitendo cha kumwambia hivyo tu alipanic na mimi nikamwambia "huo wivu ni wa kipuuzi" kusikia hivyo akapanic zaidi na kukata simu, baada ya hapo nilimchunia kidogo kwa siku tu japo si kawaida yangu, baada ya hapo.
Nikamtafuta kwa simu kwa sababu sasa tuko mbali kikazi(mikoa tofauti ) lakini hakupokea simu ila akatuma SMS kwamba"siku nzima umenisahau sababu ya huyo mdada ndo unanitafuta sasa, sihitaji simu yako " baada ya hapo nilipiga simu sana hakupokea mpaka hapo jana alipopokea na kusema haitaji mahusiano tena na haitaji tena kuolewa ila tubaki marafiki tu huku akikumbushia mambo mazito sana nilomkosea huko nyuma lakini kwa mbinde tukarudiana.
Wakuu, kauli yake imenichanganya na anaonekana hajali. Naombeni ushauri wenu sababu bado nampenda, na hata yeye tukiwa katika amani alionesha kila dalili za upendo lakini anaonekana ni mtu mwenye maamuzi magumu.