haidary hassan
Member
- Mar 9, 2014
- 69
- 5
Habari wana jamii forum,Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 20, tatizo langu kubwa ninasumbuliwa na maumivu ya mgongo pamoja na uti wa mgongo kwa takribani miaka 3 sasa, nilishawahi kutumia dawa mbali mbali za kuchua na vidonge pindi tatizo hili linanianza bila mafanikio, pia nisha Piga x-ray na kuambiwa sina tatizo lolote, cha ajabu maumivu yanaongezeka siku hadi siku na hata sijui ni maumivu ya aina gani, mgongo kila wakati nasikia hali kama ya kujinyoosha kama mtu anavyokua na uchovu, na nikijinyoosha nasikia vitu vinaachia kuanzia mgongoni, kwenye mbavu, kifuani hadi juu kwenyeshingo,wakati mwengine nasikia kama nyama zinachanika kwenye uti wa mgongo nikijinyoosha. yani situation nilikua nayo nashindwa hata nielezee vip mkanielewa and zamani wakat tatizo linaanza nilikua sisikii maumivu yoyote but now nikijinyoosha nasikia maumivu makali na haipiti hata dk 1 bila kujinyoosha coz nisipofanya hivyo nahis kama kuna vitu mgongoni vinanibana na misuli inakaza, though nafanya shughul kama kawaida lakin maisha yangu yanakua ya shida kutoka na hali, hivyo
Nilikua naomba ushaur kujua maradhi kama haya yapo na suluhusho lake ni nn.
Mkuu Kisima umeniita nimesikia ...
mkuu haidary hassan maelezo uliyotoa harakaharaka napata differentials tano lakini kutoka huo umri kuna maswali ningaliomba nikuulize..
1) Unafanya shughuli gani ?
2) Ulishawahi kuungua maradhi ya maambukizi yeyote ? mfano TB
3) Unapata ganzi ya mwili ama kuna kiungo chochote unaona kimepooza
4) Mtu akikwambia niambie wapi panauma unaweza muonesha kwa kidole exactly ni hapa "point tenderness"
5) Maumivu huwa yakuja wakati gani au ukiwa unafanya shughuli gani?
6) kupunguza maumivu huwa unafanya nini ?
7) ulishawahi kupata ajali ?
8) X ray ya mwisho ulifanya lini ? na Apart from xray ushafanya CT au MRI ?
9) Dawa gani unazotumia sasa ?
10) Unatatizo la kupumua kwa sasa?
Ugua pole
1)Mimi ni mwanafunzi hivyo Sifanyi shughuli yoyote
2)Hapana sijawah kuugua
3)Hapana hakuna
4)mara nying ni maeneo ya mfreji wa uti wa mgongo, kwenye mbavu na sometime kifuani
5)maumivu ni wakati wowote tu pind 2 nnapojinyoosha na hasa nikitoka kuamka
6)sifanyi chochote kwasababu hata nikimeza let's say panadol au dawa yoyote ya kupunguza maumivu aisaidii
7)HAPANA
8)kama miaka 2 nyuma na mbali na x-ray sijapima kipimo chochote
9)since niambiwe sina tatizo lolote sijatumia dawa zozote zaidi tu ya kufanya mazoezi kama nilivyopewa ushaur na daktar lakin sioni mabadiliko yoyote zaidi ya tatizo 2 kuzidi day after day
10)HAPANA
Oh, basi kutokana na umri wako na hilo jibu lako number 5 nakushauri kapige X ray tena ya mgongo... kuangalia nini kimebadilika ......pia itakuwa vizuri ukaenda tertiary hospital ... nina assume upo dar sasa fanya hivi...
1) nenda mwananyamala au temeke .... waeleze tatizo lako ... lazima watakwambia upige X ray tena ... baada ya kupata majibu tafuta dactari akuandikie rufaa ya kwenda muhimbili .... !! muhimbili bila rufaa utatumia pesa nyingi sana ....
kuna kaugonjwa flani kinawapata vijana chini ya miaka 40 sijui kiswahili wanaitaje ila twaita "Ankylosing spondylitis"
watu wenye huu ugonjwa wanakuwa na symptoms kama ulizoelezea number 5 ila hawa huwa wanapata maumivu ya mgongo wakiwa inactive ... na hupungua pale wakiwa active...
ukiwa umelala haupo active ndio maana ukiamka mgongo unauma sana .. as day progress maumivu yana poa...
As per books - tiba yake dawa za maumivu na kufanya mazoezi kwa sana na kama mnene punguza uzito...
ushauri
rudi for a followup x ray ya mgongo.... tafuta rufaa ya muhimbili kama upo dar ... kama upo mkoani basi nenda hospitali ya mkoa.... utabadilishiwa dawa za maumivu ... sababu sio kila mtu panadol zinamkubali ...
NOTE- Diagnosis niliyokupa sio 100% sure ...naweza nikasema ni "differential diagnosis" so usipanic brother huwezi ukamtibu au kumpa mgonjwa diagnosis through the internet .. one has to see a patient ...
pia kuna kitu mimi kilikuwa kinanikera kweli mgonjwa anakuja ana tatizo la muda mrefu lakini vyeti, all medical records kaziacha nyumbani ... since tatzio lako ni la muda mrefu beba kila kitu vyeti na x ray ya zamani kama bado unayo .......
ugua pole kaka
usiache mazoezi