Mwili kutoa majimaji (hasa mikononi na miguuni)

Mwili kutoa majimaji (hasa mikononi na miguuni)

Tayana-wog

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
28,875
Reaction score
37,657
Hodi, habari wanajamvi!!

Naomba msaada juu ya hili! Rafiki yangu ana tatizo la kutoka majimaji (yaani sio jasho la kawaida)mikononi na miguuni tu!

Kiasi kwamba hata akilala anatumia feni (Note, anaishi kusini)na mikononi hawezi hata kukushika dakika moja kashalowa!

Tatizo ni nini,au ni ugonjwa?
 
Dr. MziziMkavu unahitajika hapa plz
Mkuu Nyakwaratony sioni kuwa hayo ni maradhi mtu kutokwa na maji maji mikononi na nyayoni mimi mwenyewe wakati nina umri wa miaka 20 mpaka 28 nilikuwa

ninatokwa na majasho mikononi na nyayoni kila siku baada ya miaka fulani kupita ikaondoka yenyewe huyu.@christine ibrahim kama ana wasiwasi kutokwa na majasho mpenzi wake aende Hospitali kumuona Daktari hapa

tumesema mtu ana kuja kueleza matatizo yake wakati amesha kwenda Hospitali na hakupona ndio aje hapa

sio una maradhi unakimblia Jamii forums kuuliza hayo maradhi yako namna ya kuyatibu haito wezekana unakuja hapa baada ya Hospitali kushindikana ndio uje hapa upewe mawazo na ushauri wetu wa bure asante.
 
Last edited by a moderator:
aache sigara, bangi!
Mkuu mpinga shetani Kwani kutokwa na maji mikononi na nyayoni kunasababishwa na uvutaji wa sigara au kuvuta bangi? Mbona mimi nilikuwa ninatokwa na maji mikononi na nyayoni miaka 25 iliyopita na nilikuwa sivuti Bangi wala sigara? Maumbile ya mtu jinsi alivyo sioni kuwa hizo hoja ulizotowa ndio itakuwa ni sababu Mkuu mpinga shetani.
 
Mkuu, mpenzi wako ana:
1. Uvimbe uvimbe kwenye baadhi ya sehemu za mwili wake?
2. Kwa siku anakunywa maji kiasi gani?
3. Ana uzito na urefu gani?
4. Anatumia sana chai ya rangi, kahawa au pombe?

Nijibu maswali hayo nijuwe namna ya kukusaidia.

hodi,habari wanajamvi!!
....naomba msaada juu ya hili!....mpenz wangu ana tatizo la kutoka majimaji(yaani sio jasho la kawaida)mikononi na miguuni tu!kiasi kwamba hata akilala anatumia feni(note,anaishi kusini).na mikononi hawezi hata kukushika 1 minite kashalowa!
Tatizo ni nini,au ni ugonjwa?
 
Mkuu Nyakwaratony sioni kuwa hayo ni maradhi mtu kutokwa na maji maji mikononi na nyayoni mimi mwenyewe wakati nina umri wa miaka 20 mpaka 28 nilikuwa

ninatokwa na majasho mikononi na nyayoni kila siku baada ya miaka fulani kupita ikaondoka yenyewe huyu.@christine ibrahim kama ana wasiwasi kutokwa na majasho mpenzi wake aende Hospitali kumuona Daktari hapa

tumesema mtu ana kuja kueleza matatizo yake wakati amesha kwenda Hospitali na hakupona ndio aje hapa

sio una maradhi unakimblia Jamii forums kuuliza hayo maradhi yako namna ya kuyatibu haito wezekana unakuja hapa baada ya Hospitali kushindikana ndio uje hapa upewe mawazo na ushauri wetu wa bure asante.
Wise!sikuona kitufe cha like!unastahili like kadhaa hapa!
 
Last edited by a moderator:
Nina tatizo la kutokwa na jasho mikononi na kwenye miguu yaani napata shida sana hasa nikiwa kwenye msongamano Wa watu mfano kwenye daladala au nyakati mchana kukiwa na jua Kali.

Sasa swali langu huu ni ugonjwa? Na kama ni ugonjwa tiba yake ni dawa gani maana kwangu ni kero. Msaada Tafadhali.
 
mimi pia nina tatizo kama lako..

yani hasahasa nyakatiza mchana

ila mimi nkinawa na sabuni mikononi basi jasho hukata kwa muda
 
du kumbe tuko wengi aisee...mi huwa kama nimevaa viatu vyenye asli ya plastic basi jasho litakua ling na kama natembea kene michana nakua nateleza tu hadi kero...inanitokea nyakati za mchna haswa kipindi cha bard mwez wa 6 hadi 7 hiv
 
mimi pia nna ilo tatizo,yani nikiingia kwenye mtihani bila kitambaa,nalowesha booklet
 
Tatizo hilo analo mtoto wangu wa miezi 7 yaani nilishtuka siku anajifunza kusimama kwenye meza nikasema nimshike maana niliona anateleza sana basi kumbeba nikajua mikojo kumshika chupi haijaloana basi hadi leo nimezoea nikatamani kumpeleka hospital ila majibu nimepata hapa nashukuru sana
 
Back
Top Bottom