Wa salaam JF
Una watoto watatu umri wao juu ya miaka 15.
Ukasikia mkeo akisema kuwaambia watoto hana uhakika kama baba ni wewe au sio wewe!!
Maneno yakafika kwa ndugu na wazee wa pande zote mbili!
Likaja shinikizo la kupima DNA, utakubali kupima!? Au bora ndoa ife tu!?
(Kupima DNA ni njia ya aidha kunusuru ndoa au kuvunja ndoa!)
NB; wewe binafsi hujawahi kuhisi kuwa watoto sio wako na wala hujawahi kufikiria habari za kupima DNA!