Mussa Zungu ashauri ratiba ya SGR iboreshwe

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, ameishauri serikali kubadilisha ratiba ya safari za treni ya reli ya kisasa inayotumia umeme (SGR) kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma na kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, ili treni hizo ziwasiIi kwenye miji hiyo saa 1:30 asubuhi kwa lengo la kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.

Zungu ametoa ushauri huo bungeni jijini Dodoma na kuongeza kuwa, endapo ratiba hizo zitarekebishwa, zitasaidia viongozi wa kiserikali, wabunge pamoja na watumishi wa umma kuwahi katika majukumu yao ya kazi kwa muda unaotakiwa.

Your browser is not able to display this video.
 
NAIBU Spika Mussa Azzan ‘Zungu’, amesema kama Shirika la Reli nchini (TRC), litabadilisha ratiba za safari zake ya treni ya SGR kutoka Dar es Salaam ikafika Dodoma saa 1;30 asubuhi na pia ya kutoka Dodoma ikafika saa 1;30 asubuhi itasaidia sana kukuza uchumi.

Ametoa kauli hiyo leo muda mfupi baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kumaliza kujibu maswali ya wabunge, ambapo miongoni mwa maswali hayo lipo lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Asha Abdallah Juma aliyehoji mikakati ya serikali kuongeza safari za SGR.

Naibu Spika amesema juzi alikuwa anazungumza na kiongozi mmoja wa TRC akamwambia wana mpango wa kuleta teni itakayotumia muda wa saa 2;45 kati ya Dar es Salaam na Dodoma na kueleza kuwa hilo ni jambo la kupongezwa sana kwa Serikali ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

“Lakini nikuombe Mheshimiwa Waziri Mkuu kama wataweza kubadilisha ratiba treni zao ziingie Dodoma saa 1;30 asubuhi na ikitoka hapa iingie Dar es Salaam saa 1;30 asubuhi itasaidia sana kukuza uchumi na kuhakikisha viongozi wa serikari, wabunge, watumishi wanawahi shughuli za kiserikali kwa muda unaotakiwa,” amesema Naibu Spika.

Habari Leo

===

My Take
Hii ratiba ilikuwepo ila iliondolewa kimkakati in favour ya wenye Mabasi. Ngoja tusubirie tuone.
 
Wanasiasa wanataka kuanza kuingilia SGR kama walivyofanya kwenye ATCL, huyu ponjoro ni wa kupuuzwa tu.
 
Ni nani aliefanya utafiti Dodoma akagundua saa 12 asbh hakuna abiria hadi saa nane mchana. Yani ukikosa treni ya saa 11 asubuhi inabid ukae hadi saa nane mchana. Ukienda kwenye mabasi unakuta yamejaza...kuna kitu hapa.
Treni za mizigo zilikuja kuna ugumu gani uliopo kuanza kazi? Au watu wa Malori wanawasilisha michango yao katika ofisi za kuhujumu?

Kwa nini hakuna promo za SGR yetu kwenye vyombo vya habari kuongeza hamasa ya utumiaji.

Wekeni vivutio vya kitalii kwenye SGR, vituo vyake na njia nzima tutakuza uchumi kuliko hivyo mnavyobandika na kuonesha kila mara.

Asanteni
 
Hakukosea,walifanya hivyo Ili kuwa fursa wenye Mabasi
 
Kwa nini hakuna promo za SGR yetu kwenye vyombo vya habari kuongeza hamasa ya utumiaji.
Unaweka promo ya nini ikiwa abiria ulionao unashindwa kuwahudumia?
unataka wapige hela kupitia mgongo wa promo?
 
Ndiyo maana tukaambiwa wafanya biashara na MATAJIRI wasiwe WANASIASA
Kwann MGONGANO WA MASLAHI.
UNATEGEMEA ABOOD NA SHABIB Waipende SGR ???
 
Uchumi gani unaokua alfajiri tu.Shida ni kwamba mmehama kimwili lakini roho zenu ziko daresalama. Sgr iendeshwe kibiashara sio kisiasa na bilashaka menejimenti ya TRC imezingatia hivyo
 
Yaan ratiba zao hazijakaa kufanya biashara hata ule uendeashaji wao bado sana .
Hivi inakuwaje mfano treni kama pale dodoma kushindwa kupaki kwa wakati mmoja maana pale Kuna handaki kwa ajili ya njia ya kushukia ni kitendo cha kuongeza kipande cha reli ili kuingia ndani ya stesheni kuliko pale treni inapochelewa kutulazimisha kusubiria kwa zaid ya mpaka lisaa .
Au pale moro Kuna njia ya kupitia juu kwanini zile njia za juu zisiwekewe mazingira treni mbili zikawa zinashusha kwa wakati mmoja? Hivi tukija fika mwanza itakuwaje maaana abiria inaonekana watakuwa wengi sana kuliko kiwango
Kwan trc imeshindwa Nini kuingia mkataba na jiji Ile stendi ya shamba iliyoko mitaa ya pale stesheni isihamie hata pale kwenye magodown ya mkandarasi au kushoto mwa stesheni ili kurahisisha usafiri kuliko sasa hivi tunavolazimika kubeba na boda.
Route
Trc ipunguzwe bei ya emu na zifanye KAZI kama express train tu kutoka tsh 150,000 mpaka 90,000 na 70,000
Huku business class ya ordinary ikiwa 60,000 kusiwepo na premium kwa ordinary .
Ratiba nzuri
Dar Dom dar = 11 asubuhi(emu express)
Dar-dom-dar = saa Moja asubuhi
Dar-dom- dar= saa nne asubuhi
Dar -dom- dar = saa Saba mchana( emu express)
Dar-dom-dar= saa Tisa mchana
Dar Dom dar = saa 11 mchana( emu)
Dar-dom- dar= saa Tano usiku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…