Mugabe anaongoza kwa matokeo ya awali

mwekundu

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2013
Posts
22,477
Reaction score
21,040

Masanduku ya kupigia kura
Matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe yanadhihirisha chama cha Rais Robert Mugabe, ZANU-PF kinaongoza.Chama hicho tayari kimedai ushindi. Msemaji wa chama hicho Rugare Gumbo alisema chama hicho kilitarajiwa kushinda kiasi ya asilimia 70 ya kura hizo.

Lakini mpinzani wa Mugabe, Morgan Tsvangirai, amesema uchaguzi huo ni wa uongo na kusema udanganyifu uliofanyika una maana uchaguzi huo haukubaliki.
Waangalizi kutoka Umoja wa Afrika na jumuia ya maendeleo kusini mwa Afrika wanatarajiwa kutoa tamko rasmi hii leo kuhusu uchaguzi huo.
Mkuu wa waangalizi kutoka Umoja wa Afrika alisema tathmini yake ya awali ni kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa huru na wa haki.
source BBC swahili link Mugabe anaongoza kwa matokeo ya awali - BBC Swahili - Habari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…