Msaada:Ununuzi wa viwanja TAUSI

man dunga

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2013
Posts
3,725
Reaction score
6,580
Nimeona wanatoa masharti na vigezo vinavyokinzana.

Baada ya kulipia gharama ya maombi TAMISEMI wakatuma ujumbe kwamba lipa malipo ya awali 25% ya gharama yote halafu ndio umalizie malipo yaliyobaki ndani ya muda uliowekwa.

Lakini kipindi natuma maombi ya ununuzi kuna masharti tena yameandikwa ambayo niliyakubali, kwamba nusu ya malipo yafanyike ndani ya siku saba halafu ndio umalizie yaliyo baki.

Sasa kipi ni kipi? Si mnajua uchumi wa kujikongoja kulipa mdogo mdogo ndio mpango ili mambo mengine yaendelee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…