Msaada: Naweza kufika Namibia kwa basi?

Lugeye

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2011
Posts
1,679
Reaction score
2,917
Habari wakuu naomba msaada,

Nataka kuanza safari ya kwenda Namibia kwa njia ya basi.

Je inawezekana kwanza? Pili niwe na document zipi ili nisisumbuliwe njiani na niandae kiasi gani njiani na wanatumia hela gani huko?

Mwisho kazi gani za ovyoovyo naweza kupata fasta na mkoa/jimbo gani kuna fursa kubwa ya ajira huko Namibia?.
 
Hahaha kusafiri mpaka Namibia kwa basi pitia Zambia au Malawi mabasi mengi nauli kutoka Tz mpaka Namibia ni 150000, kuwa na dollar mfukoni, utatumia siku Tatu kufika kuhusu kazi ujipange Namibia hawaruhusu wageni kufanya kazi... Nenda swakopmund au Windhoek
 
Asante sana mkuu nimepata pa kuanzia
 
mh... ndio zile ajira za ualimu kwa wananchi wanaotoka nchi za sadc? au ni utalii wa ndani?
 
kuna tangazo la kazi lina pita humu lina toka huko namibia... sasa sijui wewe una lielezeaje lile tangazo? pili, mkuu upo namibia?
 
Namibia miaka ya nyuma tulikua tunapaita mchanga wa chuma hapachimbiki kitu...anza safari Tunduma mpaka Lusaka tsh 40,000 na ukifika Lusaka zipo bus za moja kwa moja pale intercity nauli ni kama Tsh 100,000 mpaka Windhoek kupitia Sesheke kote huko sijui Namibia,Botswana life kwa wageni kuanza ni kazi kidogo South Africa mpaka kesho itabaki kuwa kiwanja inategemeana na umejipangaje na una fani gani...Mnamibia anaitamani SA nae...
 
Safari njema mkuu.

Kufika kule itakubidi upitie Lusaka-Zambia au Lilongwe-Malawi kisha ndo upate basi za kukupeleka Namibia.
Kuhusu maeneo ya kufikia, unaweza kufikia Windhoek mji mkuu wao au ukaenda Swakopmund na Wavis miji iliyopembeni magharibi mwa nchi ikipakana na bahari ya Atlantic.

Kuhusu kazi za ovyo ovyo sijajua utafanya vipi, labda kuulizia kazi za supermarkets, vibarua vya ujenzi japo si sana kama huku.

Kama umesoma unaweza kujaribu kuulizia kazi za ofisi, bado wanaouhitaji wa wataalam. Wengi wa nguvu kazi zinazotumia brain si wazawa. Wengi ni wazimbabwe ndo wanaijenga Namibia.

Wako strict sana na issue za visa ili wakuruhusu kuingia na kukaa kwao.

Kuhusu hela wanatumia Namibia Dollar au Rands za South Africa ambayo ni one by one. Pili unaweza kwenda na US dollar utabadilishia huko. Wakati wa kubadilisha lazima uwe na passport yako na utakatwa commission % flani ya hela unayobadilisha.

Note: Kule life liko juu sana na issue ya accommodation ni expensive. Kuhusu hela wanatu
 
Mchanga wa chuma umenikumbusha mbali sana usemi huo

Ova
 

Mkuu bado Katima Murilo pako vizuri?
 
Mkuu bado Katima Murilo pako vizuri?
Mkuu pako vizuri tuu mimi truck zinapita Botswana harafu Zambia huko kwingine tulipita miaka hiyo hata Katima muliro daraja halijajengwa njia fupi ya kwenda Cape town au kutoka na gari kule maana Windhoek na Cape Town sio mbali kuliko kuitafuta Johannesburg tena 1500km..
 
Hata Uingereza unafika kwa basi. Hamna la moja kwa moja lakini.
 


Siyo Namibia tu hata Uhispania uiamua unafika kwa barabara!
 
asante sn mkuu nategemea january kuanza safari nitaleta mrejesho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…