Msaada: Natafuta fundi wa kuezeka bati Kibaha

Msaada: Natafuta fundi wa kuezeka bati Kibaha

Zainab Tamim

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2015
Posts
1,293
Reaction score
583
Natafuta fundi bati mzuri anifanyie marekebisho. Nimeezekewa bati jipya hivi karibuni na mtu aliyejifanya ni fundi lakini kaharibu.

Bati jipya kabisa, mbao mpya kabisa lakini linavuja kila sehemu na ukiliona tu unajuwa kuwa huyo alikuwa si fundi bali amenitapeli tu.

Kama kuna anaemjua fundi mzuri wa kunirekebishia, nyumba ni mpya haijesha, ipo Misugusugu, Kibaha.

Ikiwezekana hata kufumua na kuanza upya, si kitu. Mradi asinitie hasara zaidi, mabati na mbao zinazoweza kuokoka aziokoe.

Nitajaribu kuweka picha baadae.
 
Pole mkuu!!

Hivi vip siwezi kupata kiwanja maeneo hayo 1km kutoka rami!?
 
Pole mkuu!!

Hivi vip siwezi kupata kiwanja maeneo hayo 1km kutoka rami!?

Asante kaka, inatia uchungu sana, tunahangaika kujitafutia sehemu ya kujisitiri halafu anakuja mtu anaturudisha nyuma.

Viwanja vipo vingi tu, sema siku hizi bei zake.

Unataka cha ukubwa gani?
 
Mimi nimejenga Kibaha visiga nitafute kwa 0712258585 nikuinganishe na fundi aliyeniezekea. Sample ya kazi yake ipo kama utahitahi kuiona.
 
Weka picha ya roof tuione then tukushauri.
Jitahidi kupiga kutoka angle tofauti.
 
Sasa Aunt Zainab's Natural Super Clay, sasa imeonesha matumaini makubwa kwa wale wenye vipara na wale wenye matatizo ya kung'oka nywele, nywele zisizo na afya, nywele zinazokatika katika, nywele zinazong'oka kwa kutumia madawa ya nywele yenye kemikali kali, nywele zinazong'ka kwa kuvaa sana mawigi, nywele zinazong'oka baada ya kusukia nywele za bandia kwa muda mrefu.

Nimemjaribu mwanangu mwenyewe ambae alikuwa na kipara kinachokuja kwa kasi, na haya ni matokeo baada ya kutumia Aunt Zainab's Natural Super Clay kwa wiki nne tu, jionee mwenyewe: Unatokwa na Nywele? Una Kipara? Jionee maajabu ya...'
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom