Heshima wakuu,
naomba kupata uzoefu kuhusu matibabu ya wakorea hapa nchini. Nilikwenda kutibiwa nikaambiwa nina tezi dume (of course dalili wanazozisema zote ninazo). Wakasema nianze matibabu ya mwezi 1 kwa shs 150,000. Naomba mwenye uzoefu anifahamishe maana sijawahi kutumia dawa zao:
1. Je dawa wanazotumia ni za asili au za kitalaam (kuna mdau aliniambia wanatumia miti ya asili ya kwao).
2. Vipimo vyao vinaaminika?
Vipi kuhusu NIMR, maana walisema wanayo dawa kwa miezi 3 kwa sh 360,000
Naomba uzoefu wenu wakuu
Siku njema