Msaada: Dawa ya manjano kwa mtoto

Msaada: Dawa ya manjano kwa mtoto

mama grace

Member
Joined
Jan 20, 2020
Posts
65
Reaction score
297
Nimejifungua mtoto maziwa yalichelewa kutoka mtoto alipata manjano. Nilimpeleka hospital wakamuweka kwenye machine ya kutoa njano. Ninamtoa asibuhi juani ila naona bado haiishi.

Nomba mnisaidie dawa ya njano hata kama niya kienyeji nataka iishe kabisa.
 
Jua ndio dawa nzuri zaidi.

Muweke juani, kile kijua cha asubuhi kisichoumiza, hazizidi siku 5 yataisha.

Lakini je hospital walikwambia ni manjano level ya ngapi?
Je wamethibitisha shida ni maziwa pekee, isijekuwa kuna jingine(mungu akuepushe.)
 
Jua ndio dawa nzuri zaidi.

Muweke juani, kile kijua cha asubuhi kisichoumiza, hazizidi siku 5 yataisha.

Lakini je hospital walikwambia ni manjano level ya ngapi?
Je wamethibitisha shida ni maziwa pekee, isijekuwa kuna jingine(mungu akuepushe.)
Walimpima hakuna shida nyingine
 
Nimejifungua mtoto maziwa yalichelewa kutoka mtoto alipata manjano. Nilimpeleka hospital wakamuweka kwenye machine ya kutoa njano. Ninamtoa asibuhi juani ila naona bado haiishi.

Nomba mnisaidie dawa ya njano hata kama niya kienyeji nataka iishe kabisa.
Naomba kujua dalili za Ugonjwa wa Manjano tafadhali
 
Nenda Regency hosp kama uko Dar, ulizia Dr. Rahim atakupatia dawa za mwezi mzima, utampondea mtoto, ni vidonge vidogo vya njano, kwa siku mara moja, baada ya mwezi inaisha au kupungua kabisa na pia mtoto aote jua la saa 2 hadi 3 asubuhi
 
Naomba kujua dalili za Ugonjwa wa Manjano tafadhali
Homa ya manjano kwa watoto wachanga inaweza kutambuliwa kwa urahisi. Kawaida huanza ndani ya siku moja au mbili baada ya kuzaliwa na huongezeka baada ya siku 3 baada ya kuzaliwa. Njano ya ngozi kawaida huanza kutoka usoni na kisha huenea polepole kwa mwili wote.

Unaweza kuhakikisha kwa kubonyeza paji la uso ama ngozi ya mtoto kwa upole. Katika kesi ya manjano, eneo lililo bonyezwa hugeuka manjano.
 
Pole sana..

Kwa sasa, kama umanjano ulisababishwa na maziwa kuchelewa kutoka na alishawekwa kwenye mashine kwa ajili ya Phototherapy basi nakusihi kwa sasa subiri uone hali inaendeleaje.

Cha kuzingatia ni kumnyonyesha mtoto vizuri. Pia, apate mwanga wa jua ile asubuhi. Hupaswi kumfunua, mfunike vizuri utoke naye juani.

Sikilizia kwa siku mbili mpaka tatu uone maendeleo.

Vidonge vipo ambavyo utapaswa kumeza wewe kisha mtoto atapata tiba kupitia maziwa yako. Si vema sana kumnyweshwa mtoto madawa wakati hali hiyo hutokana na kutokukomaa kwa ini.

Kwa sasa acha wasiwasi. Kula vizuri na unyonyeshe mtoto ashibe. Pole sana.
 
Nimejifungua mtoto maziwa yalichelewa kutoka mtoto alipata manjano. Nilimpeleka hospital wakamuweka kwenye machine ya kutoa njano. Ninamtoa asibuhi juani ila naona bado haiishi.

Nomba mnisaidie dawa ya njano hata kama niya kienyeji nataka iishe kabisa.

Mnyonyeshe kupita kiasi…pia tumia maziwa ya SMA..yani unamnyonyesha pia unampa na formula inatoka yote…hata wangu ilikua hivyo hatukumpa dawa yoyote..ni kumnyonyesha more and more..
 
Peleka mtoto hospitalini JF hakuna MD wenye vipimo vya magonhwa kama hayo na usitumie mitishamba please huo ugonjwa ni hatari
 
Chukua hatua zifuatazo kutibu manjano ya mtoto wako:
1. Mnyonyeshe sana (Hii ndo tiba bora kabisa)

2. Mtoe juani asubuhi jua la saa 12 mpaka saa 3 na jioni jua la saa 11 mpaka linapozama,anagalau akae juani kwa nusu saa.

3. Mpe maji ya madafu vijiko 2 vya chakula mara 3 kwa siku....ukikosa maji ya madafu,Mpe maji ya miwa(Juice ya miwa) kwa utaratibu huo huo....ukikosa tafuta majani ya mti wa ukwaju yaponde ponde kisha kamua umpe mtoto kijiko kimoja kutwa mara tatu kwa siku.

Ukifanya hivyo ndani ya wiki utaona mabadiliko,njano itapungua sana au kuisha kabisa ikitegemea na level ya njano(bilirubin) aliyokuwa nayo mtoto.

Maelekezo hayo nimeyatoa kutokana na uzoefu wangu binafsi kwa watoto wangu wawili waliopata manjano siku ya 3 na 5 baada ya kuzaliwa.

Mungu atamponya mwanao MAMAGrace
 
Nimejifungua mtoto maziwa yalichelewa kutoka mtoto alipata manjano. Nilimpeleka hospital wakamuweka kwenye machine ya kutoa njano. Ninamtoa asibuhi juani ila naona bado haiishi.

Nomba mnisaidie dawa ya njano hata kama niya kienyeji nataka iishe kabisa.

Habari!
Ni vyema kwanza kutambua aina za manjano ya watoto ili uweze kusema ni nini kifanyike.

1: Machano ya kawaida/physological
2: Pathological/ya ugonjwa

Manjano hizi huweza kutofautishwa kwa:
1: kiasi cha chembechembe za bilirubini/vipimo huhitajika.
2: siku tatizo linapoanza na kuishia

Manjano ya ugonjwa huweza kuleta madhara kwenye UBONGO. Na kusababisha tatizo la mifumo ya ubongo kutokufanya kazi vyema Kernecterus.

NB: Ni muhimu sana sana kupata utofauti hapo na kupata huduma sahihi. Kosa dogo linawrza kusababisha ulemavu wa kudumu kwa mtoto. Chukua hatua, fika kwa wataalamu na vituo vyenye uwezo wa kukupa tiba sahihi.
 
Back
Top Bottom