Ndugu zangu wana jf nimeona nizungumze kidogo kuhusu wimbi hili la uchomaji wa mkaa...!!!! Ninakubali kuwa wapo watanzania wenzetu wanaoendesha maisha yao kwa kutumia shughuli za mkaa. Lakini mashaka yangu ni kasi ya ukataji wa miti na uchomaji wa mkaa uliokithiri hadi sasa..!!!
Misitu yetu inapotea ndugu zangu na hakuna tena anayefikiria nini kifanyike kunusuru misitu hii..!!! Tunayo makaa ya mawe meeengi Tanzania kwa nini tusitumie hayo katika kupikia badala ya mkaa...!!! Wenzetu nchi nyingine kama America, china na kwingineko wanatunza sana misitu na hawategemei mkaa wa mti kupikia. Tunayo gesi nyingi sana Tanzania tutumie hiyo kupikia badala ya kupikia mkaa.
Tujenge mazingira ya kupatikana gesi kwa urahisi na kwa bei ya chini ili kila mtu aimudu na au basi tuprocess makaa ya mawe ili tuyatumie kwa kupikia...!!! Hebu tusaidiane kuokoa misitu ndugu zangu. Misitu ni uhai Watanzania...!!!! Mwenye sauti na asaidie hii mbiu ifike mbali...!!!!
Misitu yetu inapotea ndugu zangu na hakuna tena anayefikiria nini kifanyike kunusuru misitu hii..!!! Tunayo makaa ya mawe meeengi Tanzania kwa nini tusitumie hayo katika kupikia badala ya mkaa...!!! Wenzetu nchi nyingine kama America, china na kwingineko wanatunza sana misitu na hawategemei mkaa wa mti kupikia. Tunayo gesi nyingi sana Tanzania tutumie hiyo kupikia badala ya kupikia mkaa.
Tujenge mazingira ya kupatikana gesi kwa urahisi na kwa bei ya chini ili kila mtu aimudu na au basi tuprocess makaa ya mawe ili tuyatumie kwa kupikia...!!! Hebu tusaidiane kuokoa misitu ndugu zangu. Misitu ni uhai Watanzania...!!!! Mwenye sauti na asaidie hii mbiu ifike mbali...!!!!