Misitu inaangamia !

kangalawe

Senior Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
132
Reaction score
20
Ndugu zangu wana jf nimeona nizungumze kidogo kuhusu wimbi hili la uchomaji wa mkaa...!!!! Ninakubali kuwa wapo watanzania wenzetu wanaoendesha maisha yao kwa kutumia shughuli za mkaa. Lakini mashaka yangu ni kasi ya ukataji wa miti na uchomaji wa mkaa uliokithiri hadi sasa..!!!

Misitu yetu inapotea ndugu zangu na hakuna tena anayefikiria nini kifanyike kunusuru misitu hii..!!! Tunayo makaa ya mawe meeengi Tanzania kwa nini tusitumie hayo katika kupikia badala ya mkaa...!!! Wenzetu nchi nyingine kama America, china na kwingineko wanatunza sana misitu na hawategemei mkaa wa mti kupikia. Tunayo gesi nyingi sana Tanzania tutumie hiyo kupikia badala ya kupikia mkaa.

Tujenge mazingira ya kupatikana gesi kwa urahisi na kwa bei ya chini ili kila mtu aimudu na au basi tuprocess makaa ya mawe ili tuyatumie kwa kupikia...!!! Hebu tusaidiane kuokoa misitu ndugu zangu. Misitu ni uhai Watanzania...!!!! Mwenye sauti na asaidie hii mbiu ifike mbali...!!!!
 
Ngoja chadema waje humu ambao wanataka kila mtu atafute hela bila kubughudhiwa wala kufuata utaratibu. Jiandae kuwavumilia.
 
Ngoja chadema waje humu ambao wanataka kila mtu atafute hela bila kubughudhiwa wala kufuata utaratibu. Jiandae kuwavumilia.

Mbona unapotosha mada mkuu? Please tulia maana hii topic ni very sensitive na haina siasa. Thanks for your understanding
 
I wish ile picha ya KILIO CHA MTI ingesambazwa tena. Ilibeba meseji kubwa sana, niliiona miaka ya tisini ngoja nijaribu kuigoogle
 
Umeleta hoja ya msingi sana kwa maana ni wachache sana kati yetu wanaoliangalia hili swala kwa uzito wake.
Ukitoka Dar es Salaam kwa barabara kuelekea Arusha, Mwanza, Kagera, Mbeya, Mtwara, Songea nk unakutana na magunia ya mkaa yanayouzwa kandoni mwa barabara kila sehemu. Hiyo ni mbali na shehena zinazotoka maeneo ya ndani ya misitu husika ambapo maloli huingia kupakia ili kuyafikisha kwa watumiaji. Sehemu nyingine zinaonekana wazi kabisa kuwa miti karibia yote imekatwa na hakuna upandaji mpya!
Swali la msingi lilikuwa ni kama serikali ingeliamua kuweka subsides kwenye gesi ya matumizi ya majumbani gharama yake isingelingana na hasara ya misitu inayopotea.
 
Ngoja chadema waje humu ambao wanataka kila mtu atafute hela bila kubughudhiwa wala kufuata utaratibu. Jiandae kuwavumilia.

Aisee...!!! Wewe ni mtanzania kweli ama mgeni...!!!! Huoni kweli misitu inavyoangami halafu unaleta siasa kweli..!!!! Chadema wananini na misitu sasa..!!?? Athari za kukata ovyo miti zinatukuta wote Mkuu..!!! Huu ni wakati wa kujadili suluhisho badala ya siasa Mkuu. Jaribu kwanza kufiki kabla hujaandika Mkuu wangu....!!!!
 
kweli tupu,mkuu miti inaondoka hivyo!
 
Jiji la Dar lina takribani watu mil4 pengine na zaid. Asilimia kubwa ya wakazi wake wanatumia nishati ya mkaa kupikia. Fanya tathmini kwa majiji mikoa na miji mingine Tz yote. Kwa wimbi la ukataji wa misitu kwa ajili ya mkaa na shughuli nyingine, upo uwezekano wa misitu yetu kupotea kabisa ni swala la muda tu!!

Mi nauliza, hivi upo uwezekano wa asilimia kubwa ya watanzania kutumia gesi au mkaa wa mawe? Kwa sababu hata wanaotumia gesi bado na mkaa wanatumia.,!!
 
wanasema tani ya moja mkaa ni sawa heka 2.5 ya miti na kwa mwaka tanzania tunatumia tani milion moja ya mkaa ni sawa heka 400,000 kwa mwaka na sawa na 1% ya misitu ya tanzani na je piga hesabu miaka 100 inayo kuja itakuwaje wakati wanasema uhai binadamu unatokana mazingira yatunze mazingira ili yakutunze lakini imekuwa tofauti tanzania saizi imechakaa sana kwas ambao wanatkiwa kusimamia misitu nao ndio wezi wakubwa mm mwenye kilio changu ni mazingira wanasayansi wanaamini hakuna mwisho wa dunia ila wanaamini mwisho wa dunia tuta uleta ss wenyewe binadamu kutokana uaribifu wa mazingira kwa jinsi tunavyo zaliana kwa kasi jinsi tunavyo zidi kuzaliana ndivyo mahitaji misitu inaongezeka wakapiga hesabu itafika miaka frani ivi kutakuwa kuna ukame sana mvua zitaanza kunyesha joto litaongezeka kutakuwa kuna shida sana kwa hiyo mwisho wadunia utatokea hivyo so wakaanzisha program ya kupunguza watu duniani hiyo program ikaanzia kwao wakasema mwisho mtoto 1 na tutunze sana mazingira kwasabau uhai wetu unatokana na mzaingira hilo kwao lika eleweka wakaangalia sehemu ambayo wanazliana sana wakagundua ni afrika ndio wakatutngenezea ukimwi mara sijui mararia yani ndio maana siku hizi magonjwa mengi sana hata uzazi wenyewe umekuwa shida sana
 
Ipo namna ya kuendelea kutumia mkaa bila kuhatarisha misitu yetu lakini walio madarakani wahatoi mwanya kwa wanaotaka kuleta mbinu mpya kufanya hivyo.

Nafikiri mpaka misitu iishe kabisa ndio tutapata akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…