Inaaminika kwamba sababu windows ndiyo os maarufu zaidi duniani hivyo inakabiliwana virusi kutokana na umaarufu wake. Zaidi ya 87% ya kompyuta duniani zina tumia winndows os hivyo basi madeveloper na madesigner wa viruses wengi wanatengeneza viruses za kurun on windows.sababu nyingine ni usanifu wa msingi wa mfumo wa uendeshaji wa os yenyewe. Windows, pamoja na DOS kabla yake, ilitengenezwa kuwa single-user os . Hii ina maana kwamba mfumo wa uendeshaji uliundwa kumwezesha mtumiaji kuwa na utawala kamili juu ya mfumo mzima. Hivyo, mfumo hauna njia ya kujua ni nani anafanya nini kwenye mfumo,na hakuna njia ya kuzuia baadhi ya watumiaji wasiweze kutawala mfumo wa comp. Kama vile, virusi wanaweza kwa urahisi kupitia mtandao bila wewe kuwa na ufahamu au kuwaruhusu.Apple Mac OSX na Linux hawakabiliwi na tatizo hili kwa kias kikubwa. Hii ni kwa sababu wao os zao ziliyoundwa kutoka chini juu na usalama katika akili, ambapo Microsoft Windows iliundwa kwa urahisi na usalama kuwa kidogo juu ya ya nani kutawala os.Mac OSX na Linux wote wanatumia filesystem ambayo nimadhubuti sana na inahakikisha ruhusa ambazo zinatokana na kila faili na folder katika mfumo zinatolewa na mmiliki wa comp, pia wanahakikisha hasa nani anaruhusiwa kufanya nini nakila file au folder. Katika Windows, kwa ili virusi viweze kuambukiza mfumo wako,ni lazima kwanza kujifanyia installation au uvifanyie installation kwenye mfumo wako. Kama ilivyoelezwa hapo awali, ni kawaida sana kwa virusi kufanya automatic installation bila ya maarifa yako au ruhusa.Lakini Mac OSX au Linux, unaweza kuwa na uwezo wa kiutawala ilikufunga au kufuta mpango flani katika mfumo wako. kwa Mac OSX au baadhi ya Linux, kama vile Ubuntu, ili ku install kitu au kufuta mpango wowote lazima kuingiza password yako. hivyo hata virus haviwezi kufanya installation bila kupewa alert ya kukutaka uingize password yako (root password) Mac OSX na Linux ni njia salama zaidi kuliko Windows - kwa sababu virusi tu hawana ruhusa ya kufanya kuinstall wenyewe nyuma ya mgongo wako. Note: hata kwenye windows 7 unaweza weka rootpassword kuzuia installation ya kitu chochote bila ruhusa yako mfano mm situmii antivirus yoyote na nimeweka rootpassword hakuna kirusi anaweza chezea pc yangu