Miaka 5 ya kifo cha Osama na rangi halisi za Mmarekani

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,638
697,929
Usiku wa siku kama ya leo miaka mitano iliyopita ndio ulikuwa wa mwisho hapa duniani kwa mtu aliyekuwa anatafutwa zaidi Osama bin Laden.

Aliyefanikisha mpango huu kwa sehemu kubwa kwenye kufichua makazi halisi ya Osama ni Dr. mpakistan ambaye aliahidiwa donge nono (halitajwi) na wamarekani pamoja na ahadi lukuki ili akubali kufanya chanjo bandia eneo lililohisiwa Osama yupo.

Wahenga wanasema penye udhia penyeza shekeli Dr wa watu maskini akaingia mkenge akawezeshwa kila nyenzo akafanikisha alichotumwa!Osama akauawa.

Leo hii ni mwaka wa tano daktari huyu anaoza kwenye jela za Pakistan wamarekani wamemtelekeza kama toilet paper baada ya kutumika.

Wamarekani wanasherehekea 5th anivessary ya kifo cha adui yao mkubwa huku mtu muhimu akiwa hakumbukwi na kawekwa kwenye makaburi ya sahau akipata mateso mengi jela.

Jipendekeze kwa mmarekani lakini tambua akishamaliza kukutumia amemaliza...haachi viporo
 
...hii issue ya Osama wakati mwingine inanichanganya tu!, wapo wanaosema Osama hakufa mmarekani muongo!,kama kweli alikufa kwanini hawakuonesha alipozikwa?!
....kwa hiyo scnario yako ya pili kuhusu huyo daktari,hapo nathibitisha kitu,sababu ilisemekana kwamba, hata huyo Osama mwenyewe alikuwa ni zao la mmarekani,km kawaida yao, wakishamaliza kukutumia kwa manufaa yao lazima wakupoteze!
 

Sijui akili yangu ikoje!,yaani naweza kuamini OSAMA alikufa lakini si kuuawa na mmarekani na wala si tarehe kama ya leo.
Kuna ukweli fulani kwenye kifo chake
Kuna ukweli kuhusu chanjo bandia ilifanikisha kupata damu ya wajukuu wa Osama
Kuna ukweli kuhusu nyumba aliyokuwa anaishi kuna ukweli kuhusu huyu daktari anayeozea jela
Kuna ukweli mchungu zaidi kuhusu wamarekani kuwatekeleza watu waliowasaidia pindi mission ikikamilika
Kuna kizungumkuti kama kweli usiku ule Osama aliuawa au alichukuliwa hai
Mwisho wa siku kuna siku ukweli utajulikana
 
Habari katika picha Osama bin Laden enzi zake za kutafutwa sana
daktari aliyefanikisha chanjo bandia(yuko lock up) asubuhi ya usiku wa shambulizi linalosemekana kumuua osama ulinzi siku zilizofuatia baada ya shambulizi Hatimaye makazi ya mtu aliyetafutwa zaidi duniani yalibomolewa na kusafishwa kabisa kuepuka kuacha alama yoyote
 
Bro mshana mimi hii habari ya kuuawa kwa Osama kama vile siiamini.

mbona umetuonesha picha za makazi yake wakati yakiwa yameshambuliwa na wakati yanabomolewa, PIA ulinzi mkali je mbona kama kweli alikuwa hatujaoneshwa japo maiti yake?
 
Bro mshana mimi hii habari ya kuuawa kwa Osama kama vile siiamini.

mbona umetuonesha picha za makazi yake wakati yakiwa yameshambuliwa na wakati yanabomolewa, PIA ulinzi mkali je mbona kama kweli alikuwa hatujaoneshwa japo maiti yake?
Sio maiti yake tuu hata mazishi na kaburi lake havipo....ikibidi mmarekani atumie na tiba mbadala kuweza kumpata jamaa
Hii pekeyake ndio nimefanikiwa kuipata
 
Sitokaa niamini kuwa huyu jamaa kauwawa na mmarekani na pia sitoamini kuwa alikufa tarehe tajwa
 
Sadam husen tulionyeshwa kila kitu mpaka wakat wanamnyonga
Jee hilo gaid la dunia hata maiti yake isionyeshwe?
Hata kabur lake?
Itachukua muda sana Mimi kuamini hilo
 
Mpaka sasa ndio ukweli pekee wenye ithibati nyingi kuwa kafa! Na kwakuwa na yeye mwenyewe yuko kimya kabisa hatoi hata video moja? Basi kwasasa inabidi tu tuamini hivyo
Yawezekana kafa ila sio tarehe tajwa mkuu na wala hajauwawa na mmarekan
Aidha atakuwa alikufa kifo cha mungu tuu
 
Sadam Hussein alinyongwa hadharani... Media zote kubwa duniani zilionesha!! sasa huyu Osama mbona yeye ishu yake ipo "classified" sana!!!

Sadam husen tulionyeshwa kila kitu mpaka wakat wanamnyonga
Jee hilo gaid la dunia hata maiti yake isionyeshwe?
Hata kabur lake?
Itachukua muda sana Mimi kuamini hilo
Kesi ya Saddam ni tofauti! Kwa kiasi kikubwa yeye alichokozwa akachokozeka lakini yeye alikuwa na address head of the state Osama was a stateless figure na akaenda kuwa tandika kwenye ardhi yao hii ni dharau kubwa sana kwa mmarekani
 
...nimeona tweets walizoposti CIA leo wakikumbuka miaka mitano toka wamuue,nikizisoma naona kama zina ukweli vile!, halafu kama alikufa kwa ugonjwa,ndugu zake/wake zake si wangesema amekufa kwa ugonjwa!, naanza kuamini muamerika alimaliza hii kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…