sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 137
*Ni Sugu wa Mbeya Mjini, akimbia ukumbini
*DC asema adhabu yake ni kumpuuza tu
MKUTANO wa kutangaza matokeo ya darasa la saba Mkoa wa Mbeya, nusura yaingia doa, baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, kupitia (CHADEMA) kulumbana hadharani na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Crispin Meela.
Hayo yaliibuka jana, baada ya kikao hicho cha kutangaza matokeo hayo ambacho kilikuwa chini ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Maria Mtunguja.
Mbilinyi alifikia uwamuzi huo, baada ya DC Meela kutoa sababu za kuchelewa kwa ujenzi wa madarasa katika Kata ya Kiwira, akidai umesababishwa na viongozi wa CHADEMA.
"Kuchelewa kwa ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari na kukosa madarasa wakati kuna wanafunzi wanahitaji kutumia madarasa hayo kuanzia Januari, mwakani (mwaka huu) ni uzembe unaosababishwa na viongozi wa CHADEMA.
"Kukwama huku kunasababishwa na wananchi wa Kata ya Kiwira, kuambiwa na diwani wao, Laulent Mwakalebule (CHADEMA), kuwa wachangie Sh 3,000 kwa kila mwananchi kiasi ambacho hakitoshi kukamilisha ujenzi kutokana na idadi ya wananchi wa kata hiyo kuwa ndogo," alisema Meela.
Bila wasiwasi DC Meela alimtupia shutuma moja kwa moja Mbilinyi kuwa akawaeleze viongozi wenzake na wanachama wake, waache kuingiza siasa katika shughuli za maendeleo.
Kwa upande wake, Mbilinyi akijibu kauli ya DC Meela, alisema katika jimbo lake lina kata 18, zinazosimamiwa na CHADEMA na maendeleo yapo.
"Namwambia DC aache kujiingiza kwenye siasa na fanyeni kazi za maendeleo ili kujenga madarasa ya wanafunzi ili waweze kuanza masomo," alisema Mbilinyi.
Lakini katika hali ya ajabu, ghafla Mbilinyi alimtolea lugha chafu ambayo hatuwezi kuiandika gazetini, kutoka nje ya chumba cha mkutano, kitendo ambacho kilionekana kuwashangaza watu waliokuwapo ukumbini.
Kikao hicho kilikuwa na wabunge, maafisa tawala wa wilaya zote za Mkoa wa Mbeya, maofisa elimu wa wilaya na afisa elimu wa Mkoa.
Baadhi ya wajumbe katika mkutano huo, walitaka mkutano huo uvunjwe, lakini wengine waliomba uendelee na kusema si kitendo kizuri mtu mmoja asababishe mkutano uvunjike.
Baada ya malumbano hayo, DC Meela alisema adhabu ya mtu kama huyo ni kumpuuza na kumwacha, kwa sababu hajui nini anachokifanya.
"Ndugu zangu mtu mmoja kama Mbilinyi, adhabu yake ni kumpuuza tu, tuendelee kujadili mambo ya msingi kwanza, tuone ni namna gani vijana wetu wataingia darasa la kwanza na wale wa kidato cha kwanza.
"Naamini kuna baadhi ya shule katika halmashauri mbalimbali, hazijakamilisha madarasa na asilimia kubwa ya shule hizi, zitakamilika mwishoni mwa Januari na wanafunzi wataanza masomo yao mwanzoni mwa Februari mwaka huu," alisema Meela.
*DC asema adhabu yake ni kumpuuza tu
MKUTANO wa kutangaza matokeo ya darasa la saba Mkoa wa Mbeya, nusura yaingia doa, baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, kupitia (CHADEMA) kulumbana hadharani na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Crispin Meela.
Hayo yaliibuka jana, baada ya kikao hicho cha kutangaza matokeo hayo ambacho kilikuwa chini ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Maria Mtunguja.
Mbilinyi alifikia uwamuzi huo, baada ya DC Meela kutoa sababu za kuchelewa kwa ujenzi wa madarasa katika Kata ya Kiwira, akidai umesababishwa na viongozi wa CHADEMA.
"Kuchelewa kwa ujenzi wa madarasa ya shule ya Sekondari na kukosa madarasa wakati kuna wanafunzi wanahitaji kutumia madarasa hayo kuanzia Januari, mwakani (mwaka huu) ni uzembe unaosababishwa na viongozi wa CHADEMA.
"Kukwama huku kunasababishwa na wananchi wa Kata ya Kiwira, kuambiwa na diwani wao, Laulent Mwakalebule (CHADEMA), kuwa wachangie Sh 3,000 kwa kila mwananchi kiasi ambacho hakitoshi kukamilisha ujenzi kutokana na idadi ya wananchi wa kata hiyo kuwa ndogo," alisema Meela.
Bila wasiwasi DC Meela alimtupia shutuma moja kwa moja Mbilinyi kuwa akawaeleze viongozi wenzake na wanachama wake, waache kuingiza siasa katika shughuli za maendeleo.
Kwa upande wake, Mbilinyi akijibu kauli ya DC Meela, alisema katika jimbo lake lina kata 18, zinazosimamiwa na CHADEMA na maendeleo yapo.
"Namwambia DC aache kujiingiza kwenye siasa na fanyeni kazi za maendeleo ili kujenga madarasa ya wanafunzi ili waweze kuanza masomo," alisema Mbilinyi.
Lakini katika hali ya ajabu, ghafla Mbilinyi alimtolea lugha chafu ambayo hatuwezi kuiandika gazetini, kutoka nje ya chumba cha mkutano, kitendo ambacho kilionekana kuwashangaza watu waliokuwapo ukumbini.
Kikao hicho kilikuwa na wabunge, maafisa tawala wa wilaya zote za Mkoa wa Mbeya, maofisa elimu wa wilaya na afisa elimu wa Mkoa.
Baadhi ya wajumbe katika mkutano huo, walitaka mkutano huo uvunjwe, lakini wengine waliomba uendelee na kusema si kitendo kizuri mtu mmoja asababishe mkutano uvunjike.
Baada ya malumbano hayo, DC Meela alisema adhabu ya mtu kama huyo ni kumpuuza na kumwacha, kwa sababu hajui nini anachokifanya.
"Ndugu zangu mtu mmoja kama Mbilinyi, adhabu yake ni kumpuuza tu, tuendelee kujadili mambo ya msingi kwanza, tuone ni namna gani vijana wetu wataingia darasa la kwanza na wale wa kidato cha kwanza.
"Naamini kuna baadhi ya shule katika halmashauri mbalimbali, hazijakamilisha madarasa na asilimia kubwa ya shule hizi, zitakamilika mwishoni mwa Januari na wanafunzi wataanza masomo yao mwanzoni mwa Februari mwaka huu," alisema Meela.