Mbowe: Bunge hili siyo halali!

Crimea

JF-Expert Member
Mar 25, 2014
24,917
33,492
Wakati Mbowe akiongea na waandishi wa habari kule Mwanza juzi alirudia hayo maneno kama mara tatu hivi,

nanukuu
"Majitu yamekaa kule Dodoma yanapanga mambo na yanapitisha kodi za kuumiza wananchi, Bunge lenyewe siyo halali halafu yanakaa yanapanga mambo ya hovyo hovyo tu"

Kauli kama hizi ni dharau kubwa sana kwa Serikali ya Mama! Ukisema Bunge siyo halali maana yake hata Rais aliyepo siyo halali vilevile.

Kwa kweli uhuru usio na mipaka wala busara ni uhuni mtupu!

Namna bwana Mbowe utakamatwa sana.
 
Achana nae Hana ishu huyo
Bunge Halali kwake ni lile ambalo chadema watakuwa 100%
 

Alichosema Mbowe ni ukweli usio na chembe ya shaka. Hata mama wa kambo hapo Magogoni mwenye urais wa urithi hilo analijua. Ushenzi, ukatili na uhayawani kwenye uchaguzi ule wote tumeushudia kwa macho yetu. Labda Mbowe aombwe asiuseme ukweli huu hadharani, kwakuwa ni ukweli unaowaumiza ccm. Na hata haya matumizi ya nguvu na kukwepa katiba mpya, ni hofu waliyo nayo ccm dhidi ya madaraka yao yasiyo na uhalali wa umma.
 
Wewe ni yapi maoni yako cremia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…