Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 1,042
- 1,305
MAPENZI NI POMBE
Kwanza yanaingia kwa utulivu kama kinywaji baridi kwenye koo lenye kiu.
Hakikuleweshi mara moja, unajiona uko sawa. Unacheka, unapiga stori, unajibu kwa utulivu.
Lakini polepole… inajikusanya kwenye damu.
Macho yako yanaanza kumtafuta bila kutumwa. Sauti yake inakuwa mziki unaoupenda kusikia kila siku.
Ukimya wake unakuwa kelele kubwa moyoni.
Na kabla hujajua umeshalewa Unashindwa kutulia bila yeye.
Unayumba bila kuguswa, unaanguka bila kusukumwa.
Mapenzi hayakuleweshi mwanzoni… lakini yakikupanda, hakuna anayekuokoa.
Na mtu hakujua kuwa moyo unaweza kulewa kwa kutajwa tu jina la mtu mmoja.
Wengi hawajui kuwa mapenzi unayanywa kama mnazi, ila yakikupanda… unamuita “baby” hata mbele ya watu wazima.
Nguvu ya mapenzi ni kubwa kuliko wimbi la bahari
Hakuna mtu wa kuyakata mapenzi ya mtu kama ambyo huwezi yakata maji
Abuuabdillah ✍️
0744883353
Kwanza yanaingia kwa utulivu kama kinywaji baridi kwenye koo lenye kiu.
Hakikuleweshi mara moja, unajiona uko sawa. Unacheka, unapiga stori, unajibu kwa utulivu.
Lakini polepole… inajikusanya kwenye damu.
Macho yako yanaanza kumtafuta bila kutumwa. Sauti yake inakuwa mziki unaoupenda kusikia kila siku.
Ukimya wake unakuwa kelele kubwa moyoni.
Na kabla hujajua umeshalewa Unashindwa kutulia bila yeye.
Unayumba bila kuguswa, unaanguka bila kusukumwa.
Mapenzi hayakuleweshi mwanzoni… lakini yakikupanda, hakuna anayekuokoa.
Na mtu hakujua kuwa moyo unaweza kulewa kwa kutajwa tu jina la mtu mmoja.
Wengi hawajui kuwa mapenzi unayanywa kama mnazi, ila yakikupanda… unamuita “baby” hata mbele ya watu wazima.
Nguvu ya mapenzi ni kubwa kuliko wimbi la bahari
Hakuna mtu wa kuyakata mapenzi ya mtu kama ambyo huwezi yakata maji
Abuuabdillah ✍️
0744883353