Mapenzi kizunguzungu

Mtoto Tajiri

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2014
Posts
300
Reaction score
173
Ni hivi bila kupoteza muda, kuna demu mmoja tulikuwa tunakaa majirani sasa ikatokea tumezoeana kimtindo baada ya miezi miwili nikiwa nimerudi home Tz maana nilikuwa pande za kati, nikiwa nimekaa kama miezi mitano hapa home Tz then nikarudi tena sasa baada yakufika kule kwasababu nyumba ilikuwa ni ya kupanga nikawa nimehamia mtaa mwingine.

Siku nikiwa nimeshaweka laini yangu ya kule nikaanza kukagua contact nikaona namba yake kisha nikaamua kumpigia kumpa hai, then baada ya hapo nikawa namtongoza lakini nilikuwa napoteza muda tu kwani sikuwa nampenda hata kidogo so nilikuwa namtania tu, lakini baada yakuwa namtumia maneno matamu matamu akajikuta ameshachanganyikiwa kabisa na mimi,vakanikubalia lakini nikataka kumwambia ilikuwa ni utani nikaogopa kumkwaza kwani angesema nachezea hisia zake, kwahiyo nilichofanya..........inaendelea

Nakuja na part2
 
Usiludi coz hio ni bongo moves kinachoendelea kinajulikana tu,acha usimalize mb zako.
 
Part2:Nilichofanya nikajaribu kuwa naye kujifanya kama nampenda ili asinistukie,kweli nikawa namtoa out sehemu mbalimbali pia namnunua zawadi flani flani nzuri coz najua jinsi yakuchagua zawadi kwa kina dada,lkn ishu ya sex nikawa napotezea kimtindo,baada ya muda kupita siku akataka apajue napokaa coz nilikuwa sijawahi kumpeleka so mwisho wa siku nikajikuta na sex nae then nikaanza kujifunza kumpenda kidogo kidogo,

lkn katika kuwa nae kwenye uhusiano nikabahatika kumsoma tabia zake na baadhi ya tabia zake ni hz:Kiburi,dharau na mgumu sana wa kuomba msamaha hata kama akijua amekosea,baada ya kugundua tabia hz nikawa najaribu kumuonya ili abadilike lkn matokea yake ndio mwendo wa kununua,mwisho wa siku nikaweka nia ya kumuacha nikaanza taratibu kukata mawasiliano na yy aligundua hilo akaamua kunitegeshea siku zake za hatari bila mm kujua kwahiyo siku nilipomwambia mapenzi basi,ndio likazuka hili la mimba,ili kuhakikisha kama kweli tukaenda kupima nikakundua kama ni kweli,nikawaza niitoe au vp?......

. nakuja na Part3
 
Mtoto Tajiri unapoelekea mwisho inajulikana ngoja nikupe ushauri kabisa.

Itaendelea part 2
 
Last edited by a moderator:
Part3:Nikawaza kutoa ni kuuwa kiumbe kisichokuwa na hatia,tukaenda kupima nikagundua kama ni kweli,kwa kuwa alishawaambia wazazi wake ikawa haina jinsi wakaniita nikakubali wito,baada ya kufika kule wakaniambia nichukue mzigo wangu kwa kuwa mila zao haziruhusu kukaa na binti wao akiwa ana mimba,nikawasihi sana wakae nae kama wiki2 ili nije kumchukua,

wiki mbili zikapita sikwenda kumchukua mwisho wa siku wakaamua kuniletea napokaa nikawa sina jinsi nikaamua kulea mimba na ss anamezaa mtoto ana miezi3,kilichopelekea kuandika uzi huu ni tabia zake:ni kiburi,anatoka nyumbani bila kuaga hata kama mm mwenyewe nipo home,akikosea hajui kuomba samahani,kabadilisha lock ya simu yake,facebook etc,

mm kuonyesha nipo tofauti nimempa password zangu zote ili aone sina kitu cha kuficha coz sina mchepuko lkn yy ameendelea na tabia zake licha ya kumuonya mara nyingi pia akikuta namba yeyote ya kike kwenye simu yangu anamtumia sms mbovu muhusika!,

Nifanyaje Waungwana????
 
hakuna cha kufanya hapo kwa sababu na wewe ni tajiri wa uzembe, masikini wa busara!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…