Salaam wakuu,
Naambatisha hapa picha ya ramani ya paa( hiddenroof) naomba wataalamu wetu wanisaidie kunipa makadirio ya idadi ya bao na mabati inayohitajika ya hiii nyumba.
Ikiwezekana pia makadirio ya ujenzi kiujumla ya kumaliza paa. Nawashukuru sana na mbarikiwe.
Fundi wako anasemaje. Navyojua mm,ukishajenga zile tofali za juu ya renta/ gata ndo fundi anapima ukubwa(m) ili kupata makadirio sahihi, na si kwa kuangalia ramani
Fundi wako anasemaje. Navyojua mm,ukishajenga zile tofali za juu ya renta/ gata ndo fundi anapima ukubwa(m) ili kupata makadirio sahihi, na si kwa kuangalia ramani
Fundi anasema atafunga mbao Alafu atakadiria mabati. Ili nisipate hasara ya kununua mabati zaidi ya inavyotakiwa.
Upande mwengine nahofia kuweka mbao Alf nikachelewa kupata mabati . Mbao zitapinda kwasababu ya jua au mvua.
Naimani ukijenga kwa kutoepuka gharama basi haitavuja. ( mfano kuweka waterproof au "kuzungushia kofia ya bati pembezoni mwa ukuta. (sijui inaitwaje kilunga ya ufundi )😀 mengine unamuachia mungu.