Sio kila idea inaweza kutengeneza valueSio rahisi kihivyo au kila mtu mwenye ideas angekuwa millionaire.
Kwa africa haya mambo ni 40% reality na 60% fantasy.
Naona kuna logicAmua tu kuondoa hiyo dhana yako: "Maisha yanachosha..." na kuibadilisha kuanzia kwenye mawazo yako na kufikiri pia kusema: "Maisha yanafurahisha sana..." ikiambatana na utendaji sahihi na kuwa na mtazamo chanja kwa mambo yote.
Pia ujue kuna ulimwengu wa roho na ndio wenye nguvu zaidi ya ulimwengu wa mwili, utumie vyema utaona utamu wa maisha. Lakini usimtumainie shetani na watu wake, bali weka nguvu za Mungu aliye hai zifanye kazi kwenye maisha yako nawe utaona utamu wa maisha.
Tough Times Never Last But Tough People Do.Hapa tusiwe ma "motivational speakers", hiko ulichoandika asimilia kubwa ya vijana tumepitia,tutapitia na tunapitia
Na hapo ulipo huwezi kujitoa wewe mwenyewe,ni UONGO
Hii ni siri niliyoanza kujifunza,unahitaji pesa,sawa?
Hakuna anayeweza kukupa pesa yake bure,eti kwa kumuelezea tu matatizo yako,probability ya watu kama hao ni almost zero
Hivi umeshawahi kujiuliza watu wanatoaje pesa?
Wape kitu kinachoongeza "value" kwenye maisha yao,njoo na bidhaa au idea yenye uwezo wa kutengeneza value kwenye maisha yao
Assume una Tsh 0.00,ila una ubongo
Fikiria kitu gani ukinambia Mimi kwenye Tsh 5,000 mkononi kitanifanya nikupe Tsh 1,000 yangu
Njoo na wazo au kitu kitakacho nipa mimi mwenye Tsh 5,000 value ya Tsh 3,000 halafu niuzie hiko kitu au hilo wazo kwa Tsh 2,000
Hapo tutakua tumetengeneza Tsh 1,000 out of nothing, na kesho nitawambia wezangu wenye Tsh 5,000 na zaidi kuhusu wewe
Huna pesa,usilalamike na kukataa tamaa,hii dunia haina huruma
Ndio maana hata binadam alitengeneza "After Life" kwa ajiri yake tu,ushawahi jiuliza "Sokwe" wakifa wanaenda wapi?
Jifunze kutengeneza pesa out of nothing, jifunze kutengeneza kitu chenye "value"
Jifunze valuable skills,kuwa best kwenye hio skill
Watu watakupa pesa tu
Ukiona maisha yanachosha, ACHANA NAYO FANYA ISHU ZINGINE TU...Duh kweli maisha yanachosha.
Naelewa.Ungeelewa nini maana ya neno "value" ingekua rahisi
Utekelezaji wa Idea unahitaji supportive environment ili idea iweze perform inavyotakiwa.Halafu kuwa na idea ni jambo moja,na kulikamilisha na jambo jingine
🤣🤣🤣👍Ukiona maisha yanachosha, ACHANA NAYO FANYA ISHU ZINGINE TU...
Sio rahisi kihivyo au kila mtu mwenye ideas angekuwa millionaire.
Kwa africa haya mambo ni 40% reality na 60% fantasy.
Ni kweli yanachosha lakini ni ajabu sana ! Hapo hapo katika Hali uliyonayo wewe ni mwenye nguvu Sana Kama unaweza kuamka asubuhi na kwenda kuchukua carton ya maji kuuza kwa abiria wanaopita barabarani kwenye mabasi.Nawasalimu,
Kuna ile Hasira iliyoko ndani yangu ya mafanikio kuna yale mawazo yaliyoko katika ubongo wangu wa namna ya kupata mafanikio, kila nikijaribu nafanikiwaje sioni njia, unakata tamaa asubuhi unajipa moyo labda leo itakuwa siku ya furaha, lakini wapi ukipita barabara unajiuliza mtu amewezaje kupata pesa mpaka akanunua pikipiki mwingine amewezaje kupata pesa mpaka akanunua gari na huyu anapataje pesa ya kujenga unakaa unafikiria inakatisha tamaa.
Unadaiwa na watu wako wote wa karibu unaona kabisa upendo wa ndugu umepungua unajihisi wewe ni binadamu usiye na akili duniani maana unashindwa kufikiria njia ya kupata pesa kama wengine wanavyopata, unaishi mwenyewe hakuna kijana mtu wa makamo hata Mzee wa kukutia moyo na kukushauri, unajihisi mpweke dunia imekuelemea, ukienda kwenye Nyumba za ibada unaona wenzako wanaenda kutoa sadaka wewe unashindwa hata kunyanyuka, unaona namna ambavyo wana ahidi michango mikubwa na mafungu ya kumi ni mamilioni ila unashindwa kutoa elfu moja maisha yanachosha.
Washikaji wanashindwa kukuonyesha hata njia au kukupa madili unaachwa na mchumba kisa unaonekana huna future (angejua yaliko kichwani) hakika asingewaza hayo yote.
Maisha yanachosha umejitahidi kusoma na mpaka sasa yule uliyemzidi elimu amepata mpenyo wa pesa ila ww huna chochote cha kuuza ukiwa na shida, Maswali kichwani hayaishi nifanye nini, nipataje pesa, nitakuwaje tajiri, nitaishi hivi mpaka lini? Nitakuja kuwa na familia siku moja itaishije kama hali yenyewe ndio hii.
Akili imechoka moyo umeondoa tumaini mbili huna nguvu, unatamani kuzima simu maana ukipigiwa simu ni mtu anakumbusha Deni lake.
Maisha yanachosha