Madai ya Katiba Mpya yametokomea wapi?

Masamila

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2014
Posts
6,506
Reaction score
7,472
Nina uhakika Mheshimiwa ambae hata yeye husema kwamba katiba mpya hakuinadi katika kampeni zake mpaka anamaliza uongozi wake 2025 hataleta katiba mpya kwa sababu hakuwahi kutoa ahadi ya katiba mpya


Wapinzani vipi? Mbona mmeniangusha!. Nakumbuka miaka ya nyuma kuna watu walitishia na kutishia kwamba hapatatosha kama JK hataleta katiba mpya
 
Madai ninayo hapa nataka niyapeleke mahakamani baadae.....
 
Endelea kusubiri shilingi in a golden plate,yanayotokea Sudan ni damu inamwagika kwa watu waoga kama mimi na wewe,yaliyotokea Kenya,SA,Ethiopia,Misri,Tunisia etc etc ni ya mashujaa kuweka rehani maisha yao kwa ajili ya kunguru kama wewe na mimi,upinzani gani uliopo hapa nchini now?kweli tunao au tunazamisha vichwa vyetu kwenye mchanga kwa kujifanya hatuoni?

Unafiki sio kitu chema hakuna upinzani ndani ya nchi yetu for now na ni JF tu ndiko kwenye freedom of expression na hatuna budi kuwashukuru kwa hili ili mimi na wewe tujifanye mashujaa wa kulalamika.
 
Mwenye nchi ameshasema hakuna katiba mpya, hana bajeti ya kuandaa katiba mpya, wala hafikirii katiba mpya ETI anachajali yeye ni matatizo ya wananchi, kama KUKUSANYA KOROSHO NA KUZIFUNGIA GALANI MALIPO hayaeleweki yanatoka lini, KUVUNJA NYUMBA ZA WAKAZI WA KIMARA KWA AJILI YA UPANUZI WA BARABARA, lakini hana bajeti ya ujenzi huo kwa sasa, unataka watanzania wafanye nini labda? Wakuu wote wa majeshi wamepewa heshima na chakula kizuri wataachaje kuua rai na kulinda watawala dhalimu? Bora kuweka kichwa mchangani kuliko kuendelea kusababisha mauaji ya raia wasio na hatia..
 
Hujaujua upinzani wa bongo? Maslahi binafsi na yasiyo endelevu ndo kipaumbele. Kwa sasa focus ni namna gani tunarudi bungeni basi.
 
Kuhusu polisi ni kweli, la korosho hakuwa na nia ya kufanya kusini iwe maskini ila alikuwa na nia ya kuifanya kusini imepende yeye maana CUF walisha anza kutishia, ila alienda kwa nguvu ya mdomo hakuwa na fedha za kuwalipa..
 
Achen yenu katba mpya muda bado tunahitaj maendeleo kwa hzo hela ya mchakato zaid ya zanat kumi,,tena mpaka,mwaka 2025
 
Achen yenu katba mpya muda bado tunahitaj maendeleo kwa hzo hela ya mchakato zaid ya zanat kumi,,tena mpaka,mwaka 2025

Tume huru ya uchaguzi, Katiba mpya Ni kikwazo kwa uhai wa chama tawala..
 
Na upinzani hawawezi kusema lolote kwani wamekwishabanwa!!!
 
Hujaujua upinzani wa bongo? Maslahi binafsi na yasiyo endelevu ndo kipaumbele. Kwa sasa focus ni namna gani tunarudi bungeni basi.
Alafu wakiitisha makongamano au mikutano kuhusu kudai katiba mpya mnawatisha na mabomu,virungu,bunduki n.k
 
Achen yenu katba mpya muda bado tunahitaj maendeleo kwa hzo hela ya mchakato zaid ya zanat kumi,,tena mpaka,mwaka 2025
Kwahiyo mlikosea kuiweka kwenye Ilani ya CCM?
 
Ni ujinga kuamini katiba mpya ni jukumu la wapinzani na si jukumu letu wananchi wote. Ujinga huu ndiyo unsyoifanya Tanzania idumae kwa kila kitu.
Hivi ni jukumu lako, langu na kila mtanzania anayejua nini maana na faida ya katiba.
 
Hii mpaka tupige ya Sudan...

CCM hii na Jiwe watoe Katiba?

Watu waoga hata mtu ukifanya kikao cha ndani cha chama mnafunguliwa eti kesi!

Yaani mtu anatawala anapata shida namna hii yanini kutawala sasa?Si heri mtu ukapumzike ulishe ng’ombe na shamba lako?!!!

Uduwanzi huu mtu una madaraka halafu unaishi kama digidigi aisee!

What a loss!
 
Watanzania hawana njia ya kupitia kudai katiba mpya walio wengi wameaaminishwa ILANI YA CHAMA ndio katiba tunayopashwa kutii na kutekeleza.
 


Mkuu ule ulikuwa ni mchezo wa kisiasa tu, ilikuwa ni kama kuwazuga watanzania. Kinachotakiwa kufanywa ni kuwawajisbisha waliofuja hela kwa kisingizo cha mchakato wa katiba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…