Hii shule ni kati ya shule zenye heshima kubwa kwa mkoa wa Iringa na viunga vyake, lakini siku za hivi karibuni imekua ni shule ya ajabu kuwahi kutoa, wizara ya Elimu, tamisemi mko wapi? Hizi shule hamna utaratibu wa kuzifuatilia? Mh. Raisi mama yetu Samia Suluhu Hassan amekuja na utaratibu wa Elimu bure kwa shule za sekondari, nia na dhumuni ni kuongeza idadi ya watoto wetu kupata elimu bila vikwazo lakini shule ya sekondari lugalo imekua ni kati ya shule zinazokwamisha harakati za muheshimiwa Raisi. Nimeshuhudia ukiritimba ambao sijawahi kuona popote, mfano sasa hivi wana utaratibu mtoto akikosea kosa lolote lile adhabu ni kupeleka trip moja ya matofali ambayo ni 200K hadi 250k lakini bado haitoshi mzqzi ukiomba utaratibu wa kuilipa hiyo pesa unaambiwa upeleke pesa shuleni kwa mkono hawakupi akaunt namba wala utaratibu rasmi wa kulipa.
Bado haitoshi endapo inatokea hauna uwezo wa kulipa pesa basi unaambiwa rudi na mwanao haijali ni mkoa gani unatoka, sawa mmeamua adhabu ni pesa je kwann isipelekwe bank? Kwanini watoto hawapewi adhabu nyinginezo zaidi ya kulipishwa pesa taslimu? Afisa elimu, katibu tawala mko wapi? Waziri tamisemi unayajia haya? Nimelipa 230k sikupewa risiti yoyote zaid ya kuambiwa mwambie mwanao arudi shuleni tena kuna walimu wana majibu machafu sijawahi kuona ndio wanaitwa walimu wa nidhamu, wamediriki kunitamkia kabisa mama hauna hiyo hela mwanao ataishia kuwa mtoto wa mtaani iliniuma sana, hakuna utu hakuna maelewano wao wanachotaka ni fedha mkononi, ukiomba akaunt unaambiwa hiyo pesa sisi tunashida nayo ukipeleka bank inachelewa kutoka.
Serikali inajua kuwa hii shule inatumia pesa taslimu na sio kupitia bank, je hamuoni kama mnaruhusu wanafunzi kubambikiwa makosa ili walete fedh mkononi zikabidhiwe kwa walimu, ukienda kwa mkuu wa shule nae anakuambia moja kwa moja kama hauna pesa ya trip ya tofali basi wewe ondoka na mwanao hawa ndio wakuu wa shule mliowapa dhamana ambao mh Rais anawataka? Nitatoa ushahidi popote, wamekataa kunipa risiti, mwanangu karudi shule kesho hata akiwa na kosa la dogo tu nitaambiwa nipeleke tena 230k.
Nimekutana na mzazi mwenzangu yeye ameambiwa apeleke mifuko 5 ya cement hivi huu ndio utaratibu wa adhabu kwa watoto? Yule mwenzangu ameshindwa kafika getini ameanza kulia, nilifanya kazi ya kumbembeleza mpaka tunafika mjini lakini hadi tunaachana alisema hana cha ziada zaid ya kusali, Tamisemi na wizara ya Elimu chunguzeni hii shule, kuna uchafu mwingi pale haiwezekani mkuu wa shule anakua mjeuri kuliko kauli za mh.Raisi, mimi bado natafuta nafasi ya kufikiaha kero yangu kwa wahusika huu ni
Mwanzo, naamini nitaokoa wazazi wengi nyuma wasio na uwezo, haiwezekani mwalimu tena mtoto ambae sawa na binti yangu anajibu kama sina 230k basi mwanangu akawe kibaka au chokoraa, walimu wana kauli mbovu, hawana UTU, wanafokea wazazi kama sisi mbwa tu.
Unaingia kwa mkuu wa shule nae hana utu kabisa anakujibu kifupi ondoka na mwanao, huyu mkuu wa shule anajua serikali inahubiri nini?
Tamisemi na wizara ya elimu chunguzeni, inawezekana ni biashara inayoanzia kwa mkurugenzi, afisa elimu hadi mkuu wa shule, haiwezekani mkuu wa shule na walimu wake wawe wajeuri kiasi kile lazima kuna uchafu unaendelea na mimi hapa ni mwanzo hii nitapeleka mbele zaidi.
AHSANTE.