Hey Guys! Poleni na majukumu.
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Hivi karibuni tumekuwa tukishuhudia matukio mengi na ya kikatili yanayohusishwa na suala zima la mahusiano ya kimapenzi.
Hivi kwa hali hii kuna mwanaume anatulia/ anamiliki mwanamke mmoja?
Nini haswa hupelekea wanaume kumiliki wanawake wengi?
Nini haswa hupelekea wanawake kuwa na wanaume wengi tukiachana na sababu ya pesa?
Ina maana suala la uaminifu limepotea kabisa?
Kuna ndoa ambazo zitafanikiwa kuwa kama za bibi na babu zetu?
Wazazi wetu walifanya nini haswa mpaka wakafanikiwa kudumu kwenye ndoa kwa muda mrefu hivyo? Ina maana hawakuwahi kusalitiana au kukoseana?