Leticia Nyerere kakurupuka

"Viongozi" wengi wanafuata mkumbo kwa matumbo yao. Inawezekana wengi tu hawaelewi kwa nini vyama vyao vinashikilia msimamo wa serikali mbili au tatu. Yaani wapowapo tu ili mradi salary inaingia hawana shida
 
Nadhani hata ndani ya CCM wapo wengi tu wanatamani wawe nje ya bunge kama ukawa but wana msimamo mmoja. Kucross party lines sio kitu chepesi. We angalia Democratic na Republicans. Nchi nyingine ukifanya hivyo unapigwa risasi.Rejea definition ya chama cha siasa, neno lengo moja na nia moja ndio basis. CCM wameshupalia Serekali 2, kuna wengi mle wangependa ziwe 3, but msimamo ni 2. Wameungana wote. Ukawa wanagawa na posho. Ruzuku na posho ndio only life line iliyobaki kwa ccm kuwaumiza wapinzani. Ndio maana walifuta Saturday na Sunday kuongeza siku. Ilikuwa strategy ya kuwafanya ukawa waone lol mahela yote hayo tunayaacha. Watu dhaifu kama Shibuda akaona ndio mtaji wa kampeni next year????
 
Bunge la katiba limenifanya kuwaelewa wabunge wenye dhamira ya kweli na watetezi wa wananchi,ni kitu cha ajabu kabisa maneno,matendo,haiba visivyoendana na umri lakini sisi wananchi ndiyo wenye maamuzi juu ya tambo zao.sisi siyo vichaka vyao.
 
Alinichekesha sana kwenye hiyo taarifa ya habari juzi hasa alipokuwa anajitetea kwamba viongozi wa CHADEMA wanamuonea eti hajawahi kusign wala kuingia kwenye vikao vya BMK, nikajua tiari dawa ishamuingia.
 
Amejishushia hadhi sana kujibu maswali kwa uelewa wa chini kiasi kile.Anataka kutuaminisha maamuzi mengi aliyeshiriki amefuata mkumbo!Kama ndio aina ya wabunge tulionao.Hatuwezi kupata katiba sahihi kwa mahitaji ya mtanzania.Naamini wapo maccm wengi wanaofuata mkumbo wa serikali mbili,japo wanataka serikali tatu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…