Kwanini siwapendi wapinzani?

Kulonganisha hoja, pua maamuzi na binge live ????? rudi shule kajifunze mwandiko
 
We ni kilaza ndio jibu ..tena oblongata wamemwagia tindikali
 
Una ujinga wa kiwango cha PHD.
 
Naanza kuamini baadhi ya tafiti za Twaweza
 
Kwa kawaida ukichukia hiki that means unapenda kile,sasa huwezipenda kitu na usiwe na unachokichukia,,,sorry hivi unauwezo wa kifikra unaojisimamia na ukafanikiwa maishani mwako.?I doubt your IQ pls! Kwani hata kwenu one family Bali kila Mtu anajinsi yake ya kuwaza na Kuishi,,,,hamuezi mkawa wote ndio mzee unless otherwise!!!!!!
 
Umedanganya kusema hauko upande wowote, kwa sababu ingekuwa hivyo usingeuchukia upande mmoja, kuuchukia upande mmoja ni dhahili kwamba unaupenda upande wa pili hivyo huwezi kusema wewe hauko upande wowote halafu ukauchukia upande mmoja. Ungesema unachukia siasa za Tanzania (Watawala na Wapinzani) wote kwa ujumla ningekuelewa kidogo na ungesema hivyo hata kupiga kura usingepiga kwa sababu hauna imani na upande wowote, lakini kusema eti hauko upande wowote na wakati umepiga kura na wakati huo unadai kuuchukia upande mmoja ni uongo wa kiwango cha 4g
 
Kuonyesha Bunge live ni jambo la msingi sana hasa wakati huu wa mabadiliko makubwa yanayofanywa na serikali kupitia Rais wa nchi.

Tusipojua yanayojadiliwa leo baada ya miaka 20 ijayo ndipo tutakapogundua kuwa tulifanya makosa makubwa sana.

Ni lazima tuwajua wawakilishi wetu na uwezo wao katika kutetea maslahi ya nchi.

Haki siku zote inapaswa iwe wazi.

Leo hii hii bunge likivunjwa halafu wakarudi kuomba kura tutawachagua watu tusiowajua. Tunawachagua wagonga meza kwa mabilioni ya fedha halafu tunakwenda kuwalipa mamilioni ya fedha.
Mimi hua nafuatilia bunge wakati wa usiku na kwenye mitandao. Kwa kweli bunge letu balikuastahili kuwa na wabunge 320 + . Wengi hawana tija kabisa zaidi ya kugonga meza na kuzomea hoja za msingi kutokana na ushabiki. Wapinzani mara nyingi wanaongea kwa mifano na hoja za wazi. Dunia ya leo sio dunia ya kudanganya watu. Baadae tutahukumiwa kwa uongo wa leo.

Ili ujue umuhimu wa Bunge live kwa wananchi basi jifunze kupitia kwa serikali ya CCM ambayo kila tukio wanalifanya live ili wananchi wawaone na kuwapongeza.
Hebu tujiulize mpaka karne hii mbunge anategemea kupata kura za wananchi kwa kwa sababu ya kugonga meza. Na wameamua kupiga marufuku bunge live sio kwa sababu ya fedha mana kuna vyombo vilikua tayari kuonyesha bure kwa gaharama zao lakini wakagundua kuwa watakaoumbuka ni wagonga meza na matusi.

Hebu tujiulize pesa za kuzungusha mwenge nchi nzima zinapatikana vipi lakini pesa za kuangamiza mazalia ya mbu hakuna?

Mwenge live unatetea vipi maslahi ya umma bila kuwa na wabunge na bunge lenye uwezo wa kuisimamia na kuishauri serikali na sio serikali kulisimamia na kuliongoza bunge .?

Wapinzani wana madhaifu yao lakini Chama tawala ndio hata madhaifua hakina mana hakiyaoni!

Hivi ni waziri gani utakayemshitaki kwa mikataba mibovu wakati ilipitishwa na Bunge?

Hivi huoni kuwa tayari watu wameshaanza kuweka wazee wa CCM wakupinga watu fulani wasiguswe japo wameanzia mbali?

Kama kweli tupo sirias kuweka misingi imara ya nchi yetu kiuchumi ,kisiasa ,
na kijamii kwa nini CCM wasitumie wingi wao kuweka mambo sawa kabla hawajapungua bungeni na kuwa wapinzani?

Hivi kitu gani kinasababisha sheria ya maadilia ya viongozi isipitiwe upya na kuwekewa misingi imara wakati huu? Nani anayeonewa huruma na kwa faida ya nani?
Kila mtu nje ya madaraka anayopewa huwa ni nafsi moja kama walivyo wengine?
Bila shaka tatizo ni CCM sio wapinzani?
Wapinzani hawana chochote zaidi ya kusema kwa kidomo!

Mwenye fedha na ushawishi ni CCM.
Jiulize inakuaje CCM imetawala zaidi ya miaka 50 lakini maendeleo ya kila wilaya na mkoa yanatofautiana sana pamoja na kwamba Kila halmashauri ina madiwani na wabunge na fungu toka serikalini?
Je tatizo ni wapinzani wakati hawana fedha za kujenga barabara?
Tangu uhuru mpaka leo bajeti ya maji na barabara ipo kila mwaka lakini bado maeneo mengi hazijafika? Je zilikua zinaishia kufanyia nini zaidi ya kutumika kwenye siasa na kuwapigia debe wabunge wasiofaa ili wakagonge meza?

Unajua chanzo cha mikataba mibovu ni siasa? Tafakari!!
 
Mtoto wa panya alimuuliza mama yake 'eti mama, mimi naitwa nani?'
Mama panya akamwambia mwanae 'ukitaka kujua jina lako nenda ukapite sebuleni binadamu wakiwepo'

Mwanapanya alipokatiza sebuleni watu wote walinyanyuka huku wakipaaza sauti zao kusema "panya huyo, panya huyo, panya huyo!!!! Na kufanya jitihada za kuutowesha uhai wake

MWANAPANYA RUDI KWA MAMIYO UMWAMBIE KILICHOKUSIBU NA JINA ULILOITIWA EENNH!!!!
 
Mm nnakuchukia saaana ww lizee !
 

Uzuri umeanza kusema ww sio mwanasiasa nasawa na mimitu
Ila kutokana na hoja yako sasa angalia kama ukiwa unataka kutoa mawazo yako kisha unaminywa usiongee na wengine wanaongea je hutalalamika?
Mfano mzuri ni kilichompata Mnyika wakati amekatazwa kuongea jambo fulani na akae kwakua mkubwa kasimama kuna aliyeropoka tens muda huohuo na hatafutwi je katika hali hiyo utakaa kimya?
Mimi sio mwanasiasa kama wewe ila nimesimama katikati,nisihukumiwe
 
Wao ndio wana roho mbaya kushawishi maandamano yanayojenga chuki badala ya maendeleo yanayoleta furaha na amani
Sababu I.Q yako haina tofauti na Lusinde au Prof Maji Marefu wapinzani wamekusamehe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…