Jamani nimekua nikifuatilia taarifa nyingi sana za jamii forum ila nilisoma taarifa za ndgu zangu walio teseka na ugonjwa wa amoeba mwaka 2012/2018 walivyokua wakielezea changamoto zao jamani na Mimi naombeni msaada Nina miezi miwili sasa nateseka ugonjwa wa amoeba nimetumia dawa kama flgly,tinidol,erthromiz,north,vumetry ,albendazol, na hata za kienyeji lakini sipati nafuu changamoto zinazo nisumbua ni mwili kubwa dhaifu na hisia ya mwili kua mgonjwa kiujumla ila sihisi maumivu sehem yoyote Ile mwanzoni nilipata choo lakini nusu kama na harisha mchanganyiko na damu ila kamasi kwa wingi nikila chakula mda huo huo napata njaa Hadi badae ndio naona nimeshiba Kuna mda na nilienda haja mda mwngine najisaidia kinyesi Cha aina ya mboga nilizokula yaani nikila mchicha najisaidia Hadi vipande vya mchicha mmeng'enyo wake sio kama siku zingine nimeeleza maelezo yasiyo ya kitalaamu naamin wataam watakuja kunisadia kwa ushauri au Nini nifanye
Pole kwa kuumwa.
Kuna vitu vya kuzingatia:
1: Historia ya kuumwa kwako haijasadifu sana mgonjwa wa Amoeba kama ni kutibiwa kwa eneo ambalo mtaalamu wa afya hawezi kupata vipimo/symptomatic treatment.
Mgonjwa wa amoeba hupata maumivu makali ya tumbo ya kukamua/kubana/cramping. Kwa siku za mwanzo utapata choo kingi cha brown na chenye harufu mbaya sana. Choo hiki huwa kinateleza sana kwa kuwa huwa na ute mwingi/does not stain the container.
Siku zinavyofuata: mgonjwa huendelea kupata maumivu makali ya tumbo na choo kiasi kidogo sana au ute peke yake ambao unaweza kuwa umechanganyika na damu. Mgonjwa wa amoeba wakati mwingine atajisikia kwenda haja kubwa na kushindwa kutoa choo chochote ingawa alijisikia kwenda kuharisha. Na hisia huonyesha kuwa unahitaji kuendelea kutoa choo kingi/tenesmus.
2: Katika maelezo yako sijaona sehemu ikieleza ulipima na kuelezwa kuwa unaumwa Amoeba.
Ni vizuri kutumia wataalamu wa maabara ili kuthibitisha ni nini hasa kinakusibu kwa kufanya vipimo vitakavyohiyajika kwa kadri unavyoumwa kuliko kutumia dawa zaidi.
3: Matumizi ya dawa kiholela
Umekuwa kwenye dawa za marudio kwa makundi yake:
A: Flaggyl na Ornidazole ni dawa za kundi moja ambazo hutibu pia Amoeba.
B: Nor T: ndani yake kuna Norflocaxin na Tinidazole. Ambazo ni dawa za kutibu Typhoid(Norfloxacin) na Amoeba(Tinidazole) ambayo bado ni lile kundi la Fraggyl na Ornidazole.
C: Kuhamia kwenye dawa nyingine ni kuusumbua mwili na madawa bila sababu. Nyingi zinabeba dawa zilezile na mwisho utajenga usugu au kusafisha tumbo lako kwa kuua wadudu rafiki wanaosaidia mmeng'enyo wa chakula. Hivyo, mfumo wa chakula kutofanya kazi yake vyema.
Mfano:
i)Heligo kit (Clarithromycin/Tinidazole) ni wale wale Erythromycin/Fraggyl/Ornidazole.
ii)Norfloxacin/Tinidazole ni walewale pia.
Kwa mazingira haya, nashawishika kusema tatizo lako la msingi laweza kuwa si Amoeba bali tatizo tofauti.
Utahitaji ushahidi mzuri ili kuhama kutoka aina moja ya dawa kwenda nyingine.
Wito:
1: Fika kituo cha afya.
2: Jieleze vyema kwa daktari kilichokutokea, dawa ulizotumia na unavyoendelea.
3: Fanya vipimo kwa kadri utakavyoelekezwa.
4: Fuata taratibu za tiba kwa kadri utakavyoelekezwa.
Matibabu mema.