Mie nawashangaa sana Jiji kwa kuzubaa hadi wakati huu kuweza kuchukua shughuli ambazo zimekuwa zikifanywa na familia ya Mzee Fisadi Kingunge. Hii wanaokusanya fedha za parking kwenye mitaa ya jijini hapa si ndio hao hao familia ya Kingunge? Kwa nini Jiji wasiifanya na kazi hiyo ili kuongeza mapato hatimaye waweze kujenga parking systems za underground na hata kujenga barabara za juu kupunguza msongamano unaokera?
Si Kingunge huyu huyu aliyekuwa kwenye Serikali ya Ujamaa na Kujitegemea? Leo kageuka jiwe kawa Bepari mkubwa anayenyonya mapato ya Taifa!