Kwenye hili suala la kuchagua mfungaji bora wa NBC PL endapo wachezaji walio vinara wa ligi watalingana magoli kwa mujibu bodi ya ligi ni kuwa msimu huu sheria zimebadilika za kuamua nani mfungaji bora.
Kwa mantiki bora ni kuwa bodi ya ligi itakaa kikao na kuamua mfungaji bora kati ya Fiston Mayele na Saidi Ntibazonkiza nani anastahili kiatu cha dhahabu, itaamua kwa kuangalia vigezo vya CAF na FIFA ili kutoa kiatu cha mfungaji bora.
Kwa msimu uliopita bodi ya ligi ilikuwa imeweka kila kitu hadharani kuwa ikiwa watalingana magoli wachezaji kwenye vinara wa ligi kuu ni kuwa atakae funga mabao machache ya penati kwenye idadi ya aliyofunga ndie mfungaji bora.
Kwa mujibu wa Bodi ya Ligi kuu ya Tanzania (NBC PL) kuelekea kuamua mfungaji bora msimu huu! Huu ndio utaratibu.
Hii siyo Mara ya kwanza kwa Tanzania ilishawahi kutokea huko nyuma Saimoni msuva aligongana magoli na mchezaji mwenzie nafikiri kuanzia hapo ndiyo Bodi ya ligi ingeweka kanuni kuhusu hili lakini Bodi ya ligi ililala mpaka Sasa.
Bodi ya ligi itaamua Nani mshindi wa Kiatu Cha ufungaji Bora kwa kujifungia chumbani pasipo na kanuni yoyote au andiko lolote la sheria/kanuni Bali watatumia ushabiki tu.
Hivyo basi watakaposema Mayele au Saidoo ndiyo mfungaji Bora watakua wametumia kanuni zipi Za mpira katika nchi yetu??
Mimi nadhani kwa kua kanuni haipo Basi wafanye Kama ilivyofanyika kwa Saimon msuva kila mchezaji alipewa kiatu Cha ufungaji bora.