Mzito Kabwela
Platinum Member
- Nov 28, 2009
- 18,904
- 7,746
Mimi huwa nasikia kuwa wakiwa kule huwa wanampiga shetani kwa mawe na lenyewe likiwageukia linawafukuza mpaka wanakanyagana wao kwa wao je hayo ni ya kweli???????[/QUOTE
Imani, Imani, Imani..................................................
wanapotupa mawe hawampigi shetani ila wanaashiria kitendo cha kumlaani shetani na Si kumpiga!
Darasa la saba utawajuwa tu,hili ni janga la taifa,bora mkasome per form one course,kuliko kupoteza mda wenu.
Vijana wa tanzania tujenge utaratibu wa kusoma na kuacha ujuaji..kila mtu anajibu naskia naskia ..ni aibu
Wakuu, Waislam wamesheherekea sikukuu ya IDD juzi na wengine jana.
Sasa nauliza, kwakuwa mji wa Mecca ulikutanisha binadamu zaidi ya Milioni Mbili kutoka mataifa mbali mbali, je ni faida zipi za kiuchumi watazipata wananchi wa Saudi Arabia kutokana na mamilioni ya wahujaji kwenda huko?
Kuna mawakala wa kuwasafirisha watu kutoka Tanzania kwenda Mecca. Nao wanafaidikaje kiuchumi?
Je, ukienda kuhiji, unaruhusiwa kuingia mtaani kufanya japo shopping ya kanzu?
Maswali mengine yanakuja....
Hakuna faida yoyote kwakua kila kitu wanapewa bure kuanzia usafiri,chakula,wakiingia madukani wanabeba zawadi waitakayo bila gharama,
Mimi huwa nasikia kuwa wakiwa kule huwa wanampiga shetani kwa mawe na lenyewe likiwageukia linawafukuza mpaka wanakanyagana wao kwa wao je hayo ni ya kweli???????
ndani ya alkaaba kumejazwa vitu gani
Mimi huwa nasikia kuwa wakiwa kule huwa wanampiga shetani kwa mawe na lenyewe likiwageukia linawafukuza mpaka wanakanyagana wao kwa wao je hayo ni ya kweli???????[/QUOTE
Imani, Imani, Imani......................... .........................
Nasikia kuna jiwe jeusi na baathi ya mabaki vitu vya zamani kabla ya uslamu kuwepo kwani hiyo alkaba ilikuwa inatumika na wapagani walikuwa walikuwa nipahala pa kutunzia miungu yao wapagani hao kabla ya uislam
Hivi kila HIJJA lazima MSIBA??? Tena wanaokufa ni wengi. This time zaidi ya mahujaji 130 wamekufa, sasa hii inakuwa toba
au balaa tupu.
Jibu sasa Wewe unayefahamu! Kwani hujamsikia hata Rais wako huwa anasema nasikia? Au nimeambiwa? Nasikia kuna mahujaji 130 wamefariki kutokana na mkanyagano wakati wakilikimbia li-shetani?!!
Hajj
Kaaba tarehe 1 Januari 2003 (wakati wa hajj)
Hajji katika Masjid al Haram mjiniMakka, Saudia
Ramani ya vituo vya haji
Haji au Hajj (Ar. حج‎😉 ni hija ya Waislamu kwenda Makka penye jengo la Kaaba. Inafanywa wakati wa mwezi Dhul-hijja ambayo ni mwezi wa 12 wa kalenda ya Kiislamu, hasa tarehe 8 - 12 za mwezi. Katika Uislamu hija hii ni wajibu kwa kila Mwislamu mwenye uwezo wa kuifanya angalau mara moja maishani mwake.
Hajj inaanza siku ya 8 ya Dhul-hijja kwa kuingia katika hali ya ihram; hii inafanywa kwa kuoga kufuatana na masharti ya dini na kwa wanaume kwa kuvaa nguo za hajj ambazo ni vitambaa viwili vyeupe pekee. Viatu
haviruhusiwi isipokuwa kandambili. Wanawake hawana masharti kuhusu mavazi isipokuwa hawaruhusiwi kufunika uso. Hapo wanaingia Makka mjini wakifanya tawaf yaani kuzunguka Kaaba mara saba. Baadaye wanaelekea kwenda bonde la Mina wanapolala katika hema zilizoandaliwa. Wengine wanatangulia kufika Mina kabla ya tarehe hii.
Siku ya 9 Dhul-hijja wanaelekea mlima wa Arafat kwa umbali wa kilomita 10 wanapokaa wakisimama na kusali hadi jioni. Baada ya machweo wanaenda Muzafila wanapolala.
Kabla ya macheo siku ya 10 Dhul-hijja wanarudi Mina ambako wanafanya ibada ya kumrushia sheitani mawe. Ishara ya sheitani inayotupiwa mawe ilikuwa nguzo ya mwamba inayoitwa jamarat lakini baada ajali nyingi ambako watu walikosa nguzo na kuwapiga wenzao kwenye upande mwingine kuna sasa ukuta. Baada ya kurusha mawe 7
wanaume wanakata nywele zote za kichwani (wanawake nywele kadhaa pekee). Halafu wanachinja sadaka maana siku hii ni sikukuu ya Idd ul Adha. Siku hizi kondoo 1 anachinjwa na wachinja wanaoajiriwa kwa kila haji.
Sehemu kubwa ya nyama inawekwa katika friza na kutumwa baadaye kwa watu maskini kote duniani.[SUP][1][/SUP]
Baadaye wanarudi Makka kwa tawaf ya pili kwa kuzunguka Kaaba mara saba. Kutoka hapa wanaenda "sa'i" wanapotembea mara saba kati ya vilima vya Safa na Marwa wakifuata nyayo za Hagar aliyetafuta hapa maji kwa mtoto wake Ismail.
Siku zinazofuata wanakaa tena Mina wanarusha mara ya pili mawe kenye kuta za jamarat.
Hajj inakwisha kwa kuzunguka Kaaba mara ya tatu na mwisho.
Mahujaji wengi wanatumia nafasi kutembela mji wa Madina baada ya hajj na kuona msikiti wa mtume.
Mwislamu aliyetimiza safari hii anapewa cheo cha heshima alhaji au hajjakwa wanawake.
Safari ya kutembela Makka nje ya siku za hajj huitwa umrah haina cheo sawa na hajj yenyewe.
Idadi ya mahujaji inaelekea kuwa milioni tatu kila mwaka. Hadi mwaka 2006 ajali nyingi zilitokea kutokana
msongamano mkubwa wa watu lakini baadaye serikali ya Saudia imeajiri wataalamu kutoka kote duniani kupanga njia salama kwa mahujaji hasa kwa kutenganisha watu wanaoelekea pande mbalimbali na njia za kufika na kuondoka. Siku hizi mahali ambako watu wengi wanatakiwa kuzunguka sehemu moja zimejengewa majengo ambako watu wanaweza kutembea kwenye ghorofa wakati mmoja.
Jewish convert to Islam does pilgrimage to plain of Arafat
Kama mtu hajui aisijitie anajua..Sasa wewe mhamiaji si utoe elimu tu? Unajua kweli matumizi ya kiswahili? Mtu akiandika "nasikia" unatakiwa umwambie iliyo kweli ili nae apate ilm murua! Kama hujui kaa kimya, kama unajua elezea we mwenye utamaduni wa kujisomea. Nini maana ya majukwaa haya kuwekwa kama c kupashana habari kwa usahihi?
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
Haya matokeo ya watoto wa darasa la saba mpaka yakitoka,tutakuwa tumesoma ujinga mwingi.Bora muende kusoma pre form one course.
Jibu sasa Wewe unayefahamu! Kwani hujamsikia hata Rais wako huwa anasema nasikia? Au nimeambiwa? Nasikia kuna mahujaji 130 wamefariki kutokana na mkanyagano wakati wakilikimbia li-shetani?!!