Kubadilika ka World Order

Kosugi

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2019
Posts
19,212
Reaction score
31,353
Wakati USA na washirika wake wakiwa bize na kuhangaika na vita za Gaza na Ukraine, China inaendelea kupanua wigo wa kibiashara na kidiplomasia kupitia mpango wake aliouanzisha wa BRI (belt and road initiative).

Mpango ambao unahusu kushirikiana na mataifa mengine katika ujenzi wa aina zote za miundombinu na kushirikiana kiteknolojia ya habari na mawasiliano na kufadhili mikopo kuendesha miradi ya mataifa washirika.

Mataifa takriban 110+ yameshaungana na huu mpango na zaidi ya mataifa 30 yamekiri kunufaika na huu mpango ikiwemo Saudi Arabia, UAE na Bosnia and Hezergovina.
 
Kila taifa lina njia zake.

China ipo hivyo unavyo iona toka kale wao biashara mbele mambo ya kujihusisha na migogoro nje ya taifa lao hawana muda nayo.

Kuna tofauti kubwa namna mchina na mzungu wanavyo fikiria kuhusu mambo mbalimbali hata tamaduni zao zinazo shape jamii zao ni tofauti.
 
Umeona yameingia Gaza???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…