Kisa cha Kweli: Sitasahau nilivyopendwa na mchawi nikaishia kurogwa

Hata usiendeleze ..cjasoma kabisa nilishuka mpaka chini kuona itaendelea nikajua walele wale nisome rubbish mtu anawaza Kichwani mwake usjichoshe kuendeleza.woi
 
Hata usiendeleze ..cjasoma kabisa nilishuka mpaka chini kuona itaendelea nikajua walele wale nisome rubbish mtu anawaza Kichwani mwake usjichoshe kuendeleza.woi
Hakuna aliyekuita, anayekuomba wala kukulazimisha kusoma.

Hutaki kusoma unaacha, hakuna anayekuomba kusoma. Na story itaendelea hadi mwisho na hakuna chochote utafanya.

You're not that important.
 
Yamoto
 
Inaendelea sehemu ya tano.

Nilitembea moja kwa moja hadi getto, nikafika nikajilaza kichwa kilikuwa kina mawazo mengi sana. Naamini watu wengi ambao nilikutana nao njiani inawezekana walibaini siko sawa. Nilikaa sikuwa hata na nguvu ya kupika, nilikuwa nawaza tu. Baadae washkaji tuliokuwa tunakaa nao getto walirudi kutoka shule ilikuwa mida ya saa tisa hivi. Jamaa walilalamika kwa nini nimewahi kurudi kutoka shule lakini sijapika,nikawaambia naumwa. Jamaa walipika ugali dagaa nikala kidogo kwa kujilazimisha. Baadaye nikaona nimfate Vumilia getto kwake ili twende alikokuwa anasema, niliona siwezi kusubiri wakati niko kwenye mdomo wa Simba.

Uzuri alipokuwa anakaa haikuwa mbali sana, nilitembea kwa dakika kadhaa chache nikawa nimefika. Nilibisha hodi akafungua mlango nikaingia ndani. Nilivyoingia, nikaketi chini kwenye godoro lililopo chumbani kwake, nikawa namtazama. Nilimuona kama mtu aliyekuwa amebaki kama tumaini langu la mwisho. Moja kwa moja, nikamwambia twende ulikokuwa unasema. Alikataa akasema nitakuja kukuchukua mwenyewe usiwe na haraka. Nilimbembeleza lakini alikataa katakata akasema atakuja baadae usiku. Niliamua kurudi getto, nikafika nikalala nikimsubiri aje anichukue. Ilifika hadi usiku saa tatu alikuwa hajaja, nikajikuta nimepitiwa na usingizi. Baadae nilishtuka usingizini, kuna mtu alikuwa kama ananivuta mkono. Niliangalia na kumkuta alikuwa mtu ambaye amevaa nguo nyeusi tii, nilipiga kelele kwa nguvu hadi mshikaji wangu mmoja aliyekuwa amelala akashtuka kutoka usingizini. Mshikaji mwingine alikuwa mezani amewasha kibatari anapiga kitabu naye aliniangalia, akaniuliza.

"Vipi unaota?"

Nilimtazama Yule mtu na kugundua alikuwa ni Vumilia. Usoni alikuwa amepaka dawa nyeupe za unga unga. Alinifanyia ishara ya kuniambia nikae kimya. Kilichonishangaza licha ya kwamba Vumilia alikuwa pembeni kidogo tu ya jamaa anayesoma mezani lakini mshikaji alionyesha haoni chochote. Ilikuwa ni kama mimi tu ndiye niliyekuwa namuona. Alinifanyia ishara nisimame, niliwaza kidogo kuona kama nachokifanya ni sahihi. Ghafla kuna wazo lilikuja kichwani likaniambia hivi kwa nini nimemuamini Vumilia ghafla, je kama ndio yeye anataka kunichukua kunipeleka kwa wachawi wenzie wakanimalize, si ndio naenda kufa kirahisi rahisi tena kwa kujipeleka mwenyewe. Wazo hili lilianza kama utani lakini lilinishawishi, nikajikuta natikisa kichwa kuashiria kwamba nimekataa na sikuwa tayari twende naye. Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu.

"Vipi umeogopa, au unadhani nataka nikufanyie kitu kibaya, kumbuka nilikuambia uwe jasiri" aliniuliza kwa sauti kubwa

Nilipigwa butwaa na kumuangalia mshikaji aliyekuwa anasoma, lakini macho alikuwa amekodolea kwenye kitabu, ni wazi hakusikia chochote. Nilishangaa nikajisemea moyoni ama kweli duniani kuna mengi. Nilikaa kimya kwa kuogopa nikijibu jamaa angesikia na kuanza kuwaza tofauti.

"Sikia nikwambie mr the dragon, hata hapa nimefanya ustaarabu tu. Ningeamua ningekuchukua kimya kimya hadi ninakotaka kukupeleka bila wewe kujua. Hujiulizi jana umepelekwa makaburini na kuchanjwa bila kujitambua, sasa nikitaka kukupeleka unadhani nitashindwa. Kama hauamini subiri"

Aliongea vile na kuanza kurudi kinyumenyume hadi kwenye kona moja ya chumba na kupotea. Sijui kilitokea nini lakini nilijikuta nashikwa na usingizi mzito ghafla na nilipokuja kushtuka nilijikuta nilikuwa nje ya ile nyumba, Vumilia akiwa pembeni yangu amenishika mkono.

"Umeamini sasa kwamba naweza kukupeleka popote. Sikiliza Mimi napambania maisha yako kwa hiyo fuata kila nitakachokwambia"

Mpaka hapo sikuwa na ujanja zaidi ya kutii amri, niliamua sasa liwalo na liwe. Vumilia alinitangulia na kuniamuru nimfate kwa nyuma. Alianza kutembea kwa miguu halafu mimi nikawa namfata kwa nyuma. Tulitembea kwa mwendo wa dakika chache tukawa tumeshafika kijijini kwetu. Yalikuwa ni maajabu yaani sehemu ambayo huwa tunatembea sio chini ya masaa mawili na nusu tulitembea kwa dakika zisizozidi kumi na tano.

Tulipofika kwenye kijiji chetu alininong'oneza "tunaenda kwa mzee Nkelebe"

Mzee Nkelebe alikuwa ni mganga maarufu wa kienyeji pale kwenye kijiji chetu.

Tulipiga hatua ndani ya dakika chache tulikuwa tumeshafika.

Itaendelea kesho asubuhi!

Leo nimeandika kwa kifupi kuonyesha bado tuko pamoja maana watu washaanza kupata wasiwasi, kwamba sitamalizia. Jamani niko hapa mwanzo mwisho.

Na kesho ni weekend nina muda mwingi wa kuandika kwa hiyo ni bandika bandua.

Usingizi nipumzike. Good night
 
Hakuna aliyekuita, anayekuomba wala kukulazimisha kusoma.

Hutaki kusoma unaacha, hakuna anayekuomba kusoma. Na story itaendelea hadi mwisho na hakuna chochote utafanya.

You're not that important.
Mtu anayeandika story yake na kushare huwa namkubali sana. Kwasababu
1. Ametumia muda wake kuandika. Watu hufikiri hauna kazi, wewe ni kuandika na kuweka tu na wengine wanalazimisha
2. Unasoma bure
Ndiyo maana nikikuta nasoma, nisipokuta siwezi kulalamika maana kwa jicho la tatu nilitakiwa nikupe hela ndiyo maana watu wanaweka Youtube. Kuna wale hufikiri kama story anatoa Mello, watakulazimisha.
Big up sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…