Kuna vifaa tofauti vya kupimia moyo, lakini kitu muhimu sio tu kupima bali kujua kusoma matokeo.
Na unatakiwa kupima ukiwa umetulia kwa muda kabla ya kupima
Cha kwanza na nadhani ni rahisi kupata hapa bongo ni kipimo cha msongo wa damu, hiki kitaonyesha kama mapigo yako ya moyo yanafanya kazi ya kusukuma damu mwili katika hali ya afya salama ya moyo.
View attachment 3552696
Majibu yanayoonyeshwa ni majibu mawili ya Systolic yaani nguvu ya moyo kusukuma damu kwenye mishipa(Namba kubwa) na Diastolic yaani nguvu wa damu wakati moyo uko kwenye mapumziko kati ya kila msukumo(Namba ndogo)
Hivi ni vishiria vya kama pressure kama tunavyosema iko juu au iko chini
Majibu ya 120 -130 (Kubwa)/80-90 (Ndogo), mapigo yako salama na moyo unafanya kazi vizuri.
Majibu ya Kuanzia 140/100, na kwenda juu hapo ndo wanasema una pressure kubwa na unatakiwa kumuona daktari wa moyo, sio vilaza wa dispensari.
Na vipimo vikionyesha 90/60, sio mbaya kama ni mwana michezo au ni mu wa mazoezi, lakini kama sivyo haya majibi yanaweza kufanya unasikia kizunguzungu na kujisikia umechoka sana
Angalia hapa viwango vya vipimo na maelezo yako ambayo nadhani utayaelewa baada ya ufafanuzi niliotoa
View attachment 3552697
Siku hiz kuna saa janja hasa Apple, Samsung na Huwaei zinapima moyo kwa ustadi mkubwa ila ndio bei zake sasa, lakini sikushauri ununue za kichina bora ununue hiko kifaa nilichoweka hapo juu.
Kuna vifaa tofauti kama ECG ila hii ni ya kitaalamu zaidi na unashauriwa ifanyike hospitali tu au Heart Rate monitor ambazo hata saa janja nyingi zinakuwa nazo lakini majibu yake sio ya kuamini