Kingwangala waziri bora awamu hii!

10mil

Member
Joined
Jun 14, 2019
Posts
64
Reaction score
79
Wakuu kwa mawaziri wa awamu hii nadiriki kusema waziri wa mali asili na utalii ni wazuri anayeonekana anajua anachokifanya,tangu aingie kwenye hiyo wizara ametulia vizuri na amekuwa mchapakazi.

Kila mda yupo kazini,hakuna siku hutamwona akiwa kazini kwenye mbuga na sehemu zingine zinazohusu utalii,ameleta mabadiliko na ameendana na kasi ya mheshimu Rais.

Haya ni maoni yangu,je ni waziri gani mwingine ameonyesha jitihada?
 
Kwa kuchonga Sanamu ya Kwame Nkurumah badala ya Hayati Baba wa Taifa hili.
 
Sanamu ndio inakosesha... usingizi. Uoga wa nini?

Nilimsikia Naibu Waziri wake aiseee yupo vizuri sana kwenye mengi aliyatamka siku Waziri wake juzi akiwa mgeni rasmi.
 
Hana ubora wowote huyu. Acha kusifia watu wasiostahili.

 
Kuongoza watanzania ni kazi rahisi sana.

Fanya vituko vituko tu, vaa maviatu na magwanda ya askari wa wanyamapori,kimbiakimbia hovyo huku ukihakikisha unapigwa picha. Hapo unakuwa mchapakazi na bora kabisa.
 
jamaa ndiye waziri pekee anayeeleweka , afu ni mjanja hajikombi kwa jiwe ile ya kupitiliza kama wengine
 
Hapana,mimi namuona January Makamba na Jaffo kama waki vizuri zaidi!
 
Kila mda yupo kazini,hakuna siku hutamwona akiwa kazini kwenye mbuga na sehemu zingine zinazohusu utalii,
Wewe ni observer wa kiwango cha awamu ya 5, najua unamwona yuko kazini kupitia account zake za mitandao ya kijamii au kuna njia nyingine tofauti na hiyo?!
 
Rais ndio anajua nani bora nani sio bora kwa kuwa ndiye aliyewateua kwa vigezo vyake na anatumia vigezo hivyo kuwapima.

kila muda kufanya kazi si kigezo cha kusema fulani ni bora, inawezekana unafanya muda mwingi kazi kwa sababu huwezi kufanya kwa muda mchache. Hii inanikumbusha kipindi cha shule, wengine walikuwa wanatoboa wanasoma na wengine prepo tu ikiisha wanaenda kula na matokeo ya wanaotoboa yanakuwa si mazuri. kwa hiyo hapo tunaangalia matokeo.
 
Rais ndio anajua nani bora nani sio bora kwa kuwa ndiye aliyewateua kwa vigezo vyake na anatumia vigezo hivyo kuwapima.

kila muda kufanya kazi si kigezo cha kusema fulani ni bora, inawezekana unafanya muda mwingi kazi kwa sababu huwezi kufanya kwa muda mchache. Hii inanikumbusha kipindi cha shule, wengine walikuwa wanatoboa wanasoma na wengine prepo tu ikiisha wanaenda kula na matokeo ya wanaotoboa yanakuwa si mazuri. kwa hiyo hapo tunaangalia matokeo.
 
Ubora wake umeonekana kwa kusafirisha wanyama kwenda chato? Angalia mafanikio katika nyanja ya msingi kwa mfano je ameweza kuongeza idadi ya watalii ukilinganisha na mawazor waliopita au ameweza kuondoa changamoto wanazopata watalii wanapotaka kutalii
 
Hakuna kitu hapo. Kwanza aombe msamaha kwa ile sanamu inayosemekana ni ya Baba wa Taifa wakati haina hata chembe ya sura ya Baba wa Taifa. Angekuwa makini asingefanya kosa hilo
 
Labda kwa vile kila wakati yuko na makamera ndio sababu unamuona bora! Au kwa kuwa 'ameumba' mbuga ya wanyama nyumbani kwa mtukufu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…